Jumanne, 3 Septemba 2013

ZAMALEK WANTED IT MORE - TOLAN



Kocha mkuu wa Zamalek Helmy Tolan ameelezea kufurahishwa kwake na matokeo ya ushindi ya magoli 2-1 dhidi ya Orlando Pitares wakati wa mchezo wao wa makundi ya ligi ya mabingwa barani Afrika.

Tolan amesema kuwa haikuwa kazi rahisi kwa wao kuchomoza na ushindi ukizingatia wapinzani wao wanatimu nzuri zaidi ya kikosi cha Zamalek hata hivyo jitihada za vijana wake zimewawezesha kuchomoza na alama 3 muhimu kunako mchezo huo.


Endapo Zamalek wangepoteza mchezo huo ingekuwa ndiyo tiketi ya wao kuyaaga michuano hiyo lakini ushindi wa magoli 2-1 unaibua matumaini mapya kwa kikosi hicho kusonga mbele katika mechi zingine zilizosalia.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni