Wauza mitumba wa ilala Un colonized never say die
titi munda mtwale wa kuchwela watoto wa jiji Ashanti united wanakaba kayeka
wameonesha nia ya kutaka kumsajili nahodha na mlinda mlango namba moja wa timu
ya Taifa ya Tanzania Taifa stars Juma K Juma, Juma Kaseja.
Ashanti United inayodhaminiwa na kampuni ya S.S.B
kupitia kinywaji chake cha Azam Malta kimetangaza dhamira hiyo kuelekea kwenye
dirisha dogo la usajili ambalo linataraji kufunguliwa November 15 hadi Disemba
15 mwaka huu.
Katibu mkuu wa Ashanti Abubakar Silas amesema kuwa
ndoto kubwa ya Ashanti ni kutaka kumsajili Juma Kaseja ambaye ni mchezo mkubwa
hapa nchini mwenye uzoefu wa kutosha wakiamini atakuwa na msaada mkubwa
kuiwezesha Ashanti kufanya vizuri kwenye msimu huu wa Ligi.
Silas amemtaka Kaseja kuwatazama Ashanti kwa jicho
la tatu kwakuwa nib ado timu changa na haina uwezo wa kutosha kumsajili kwa dau
kubwa litakaloendana na hadhi yake.
“Sisi kama Ashanti United kwa mtu kama Kaseja
anaweza kusaidia sana siyo siri, kwa mazingira yaleyale tulomchukuwa Said
Maulid tunaweza kumchukuwa Kaseja unajuwa katika mpira kila samaki ana price
yake
“Kaseja ni mchejazi mkubwa ni Tanzania one, price Tag
yake ni kubwa sasa yeye binafsi kama alivyoonesha nia SMG na yeye afanye hivyo
hivyo”
“Iwapo atakuwa tayari sisi tunamtaka Kaseja
ijapokuwa hatuna pesa za kumlipa”
Kwa upande wake Juma K Juma amewatoa hofu Ashanti
United pamoja na kuwataka wakae kwenye meza ya mazungumzo pamoja nae ili kufikia
muafaka wa kuipata ridhaa yake kuitumia klabu hiyo kwenye msimu wa 2013/2014.
“Kwanza wanatakiwa wakae na mimi wasiniogope
wanatakiwa kwanza waniite mimi tukae tuongee then wanisikie wanaweza wakawa
wananiogopa kumbe ikawa tofauti na wanavyofikiria”
“Kuna timu ambazo unaweza kwenda kucheka tu kwa
kujitolea timu kama Ashanti ni ya kujitolea kikubwa wakae na mimi wafanye
maongezi bado nawapenda mashabiki wangu waendelee kunisupport Inshaallah Mola
ataleta kheri yake.”
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni