Jumatano, 18 Septemba 2013

KIM PAULSEN AIZUIA TAIFA STARS KUCHEZA DHIDI YA IRAN

Kim Paulsen
Kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania Taifa stars amelazimika kuizuia timu yake kucheza mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Iran mwezi Octoba kutokana na wachezaji hao watakuwa kwenye vibaru na klabu zao zinazoshiriki ligi kuu ya Tanzania bara.
Mbali na ligi kuwa inaendelea pia Stars amewataka wachezaji wake wawe na muda mwingi kwenye vikosi vyao kabla ya kuwaita wachezaji hao kuunda timu ya Kilimanjaro stars itakayoingia kambini kujiandaa na michuano ya Challenge

Stars kwasasa imevunja Kambi baada ya kushindwa kuvuka vikwazo vya kutinga fainali za kombe la dunia mwakani nchini Brazil.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni