24/09/2013:
KAMPUNI
kubwa duniani yenye utaalamu wa kuwezesha uhamisho wa fedha kwa njia ya mtandao
(online) ya Timesof Money, imedhamiria kuingia katika soko la Tanzania, kama
sehemu ya mpango wake wa upanuzi barani Afrika.
Katika mpango wake huo, kampuni hii yenye makao yake
makuu jijini Mumbai nchini India, inatajaria kuzindua mpango/mfumo wa kutuma
fedha nchini toka kwa Watanzania walioko nje ya nchi (remittance) kwa njia ya
mtandao (Online). Mfumo huo ambao
unatarajiwa kuleta mapinduzi makubwa nchini, utawawezesha Watanzania
kupata/kutuma fedha kutoka mahali popote duniani moja kwa moja katika akaunti
zao za benki, kadi za malipo ya kabla (pre-paid cards) pamoja na simu zao za
mkononi.
“Katika mkakati huo huo wa kijitanua barani Africa,
hivi karibuni tumeingia mkataba na Benki ya Diamond Trust nchini Kenya kutoa
huduma kwa wateja wake wa mfumo wa ‘NationHela’,” alisema Afisa Mtendaji mkuu
wa TimesofMoney, Avijit Nanda.
Kwa mujibu wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano
wa Kimataifa wa Tanzania, idadi ya Watanzania wanaoishi na kufanya kazi nchi
mbalimbali duniani/ughaibuni (diaspora) inakadiriwa kuwa zaidi ya million
mbili. Na kwa mujibu wa ripoti ya Benki ya Dunia, inakadiriwa kuwa Watanzania
hao waliingiza nchini kiasi cha shillingi billion 120 (US$ 75million)mwaka
jana. Kwa kutumia huduma hii, Watanzania wanaoishi nje ya nchi wataweza kutuma
pesa kwa jamaa na marafiki zao nyumbani, hivyo kuondoa usumbufu wa kusimama
katika foleni kwa mawakala wa kuhamisha fedha.
"Idadi ya raia wa nchi za Afrika Mashariki na
hasa Tanzania wanaoishi nje ya nchi zao inaendelea kuongezeka na hii ina
maanisha uhitaji wa kutuma fedha nyumbani (remittance) pia unaongezeka. Ni kwa
sababu hii tumeona kuna umuhumi wa kuingia katika soko hili. Tukiwa na
teknolojia ya kisasa, tunatoa ahadi ya huduma bora kwa kutumia wataalamu wenye
uzoefu mkubwa katika nyanja hii,” alisema Bw Nanda.
Bara la Afrika linakadiriwa kuwa na idadi ya watu zaidi
ya million 30 wanaoishi nje ya nchi zao za asili. Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo-- International
Fund for Agricultural Development (IFAD), unakadiria kwamba mwaka jana (2012)
wahamiaji hao kwa pamoja wamechangia/ wametuma kiasi cha dola za marekani
millioni 38.6 katika fedha kutoka nje, kwa familia na jamii zao nyumbani.
Hata hivyo, moja ya kikwazo kikubwa kwa ukuaji wa
mtiririko kutuma fedha nyumbani (remittance) katika nchi za Afrika hasa zile
zilizopo Kusini mwa jangwa la Sahara, ni gharama kubwa ya kutuma fedha. Wastani
wa gharama ya kutuma fedha kwa Afrika ni karibu 12 % ya juu kuliko wastani wa
kimataifa wa 8.96 % na karibu mara mbili ya gharama ya kutuma fedha kwa Asia ya
Kusini.
"Gharama kubwa za ada zinazotozwa na makampuni
na mawakala wa kuhamisha fedha barani Africa, imekuwa ni kikwazo na imeathiri
mtiririko wa kuingiza fedha toka nje ya nchi. Mtumiaji wa mwisho ndiye
anayeathirika na kubeba mzigo wa gharama/ada kwa kiasi kikubwa. Kwa kupitai
mfumo wa mtandao (online-transactions) tunatarajia inaweza kusaidia
kupunguza gharama hizi kwa kiasi kikubwa, jambo ambalo litatao ahueni kubwa kwa
mtumiaji wa mwisho,” bosi huyo wa TimesofMoney alisema.
Kuhusu TimesofMoney :
TimesofMoney ni kampuni inayoongoza duniani
kwa kufanya biashara ya uhamisho wa fedha kitaalamu. Kampuni hii
inisifika kwa kufanya biashara na wateja mbalimbali wakiwemo wa rejareja
na kitaasisi duniani kote.
Ikiwa imeanzishwa mwaka 2000, TimesofMoney, inatoa
ufumbuzi wa mifumo ya malipo kwa wafanyabiashara.
Huduma zinatolewa duniani kote - kuwezesha uhamisho
wa fedha watu kwenda kwenye nchi zao za nyumbani na kutoa huduma ya urahisi wa
kutumia internet au simu.
Ikiwa na zaidi ya miaka 12 ya uzoefu, TimesofMoney
inajivunia mahusiano mazuri na ya nguvu na wateja wake wakiwemo wale wa
rejareja, kitaasisi na pia inaheshima na mafanikio makubwa katika sekta ya
fedha kwa miaka kadhaa sasa.
Kampuni hii pia inajuvunia kuwa mbia mkubwa (kuwa na
hisa kubwa) katika Mtandao wa Kimataifa, na ni kiongozi wa soko katika mfumo wa
malipo. Inasimamiwa na timu ya wataalamu wenye uzoefu kutoka benki na historia
nzuri ya fedha.
Maelezo zaidi zinapatikana kwenye tovuti ya kampuni www.timesofmoney.com .
Kwa
maswali wasiliana na:
Lucy T. Ngongoseke | Tabasamu Public Relations |
(Mobile) +255 754 602674 | lucy@tabasamupr.co.tz
Bhavin Shah | TimesofMoney | (Desk) + 91-22-3098
8491 | bhavins@timesofmoney.com
Mike Omuodo | H+K Strategies | (Mobile) +
254-720910146 | Mike.Omuodo@hkstrategies.co.ke
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni