Alhamisi, 12 Septemba 2013

KAMATI TENDAJI YAJIKAZA KIUME HATIMAYE YATHIBITISHA PATRICK NAGGI NI MIONGONI MWA SECRETARIETY


Sanga, Katabaro kulia nae ndani
Kamati tendaji ya mabingwa wa ligi kuu Dar es Salaam Young Africans imeshindwa kuficha ukweli juu ya ujio wa mkenya Patrick Naggi na hatimaye hii leo imemtangaza kuwa miongoni wa wajumbe wa secretariety ya Yanga.

Awali ujio wa Naggi ulihusishwa kuwa amekuja kuchukuwa mikoba ya Lawrence Mwalusako anaekaimu nafasi ya ukatibu klabuni hapo huku ikizua mtafaruku mkubwa.
Sanga akitema cheche

Baraza la wazee la Yanga lilikuwa la kwanza kupinga ujio wa Naggi wakisema kuwa hawamtambui na wala hawatambui nafasi yake.
Wazee wote kimyaaaaaaaaaaa

Makamo mwenyekiti wa Yanga Clement Sanga leo alimwaga mchele kwenye kuku wengi akisema kuwa ujio wa Naggi pamoja na viongozi wengine wawili kwenye secretariety unalenga kuongeza nguvu klabuni hapo na wamewapa miezi miwili kuwatizama na baadae kutangaza rasmi nafasi zao.
Hao ndo wajumbe wapyaaa Naggi kulia, katikati mshauri pembeni kule mjumbe

Je wewe hii umeielewaje??????????????????????????

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni