Alhamisi, 5 Septemba 2013

MICHEZONI



Kocha mkuu wa Kenya The Harambee stars Adel Amrouche amevunja ukimya na kwanza mara ya kwanza ameiomba serikali ya nchini humo kuisaidia timu yake kuelekea kwenye mchezo wao wa wikiend hii.
The Harambee stars kwasasa ipo kambini ikijiwinda dhidi ya Namibia katika mchezo wa kuisaka tiketi ya kushiriki fainali za kombe la dunia mwakani.
Adel ameitaka serikali kuwapa ari wachezaji pamoja na kujitolea muda wao mwingi kuwahamasisha wananchi kuipa nguvu timu yao ya taifa.
Kocha huyo amewataka wadau wengine kujitokeza kutoa ahadi katika kikosi hicho ambacho kinatawaliwa na wachezaji wenye umri chini ya miaka 25.
FIFA DELAY SENEGAL-UGANDA BY AN HOUR
Shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA limefanya mabadiliko ya muda kwenye mchezo wa hapo kesho kati ya Senegal na Uganda ukiwa ni mchezo wa mchujo wa kombe la dunia 2014.
Mechi hiyo itapigwa Marakesh nchini Morocco, kuanzia majira ya saa 3 usiku kwa saa za Morocco badala ya saa 4.
Rais wa Shirikisho la soka la Uganda Edgar Watson amethibitisha kupokea taarifa hizo kutoka FIFA hata hivyo hawajafafanuliwa sababu za mabadiliko hayo.
Senegal wanaongoza Kundi J wakiwa na alama 9 wakifuatiwa na Uganda wenye alama 8.
BAFANA V ZIM SET FOR ORLANDO
Mchezo wa kimataifa wa kirafiki kati ya timu ya taifa ya Afrika kusini Bafanabafana na Zimbabwe uliopangwa kupigwa September 10 mwaka huu, imebainika utaunguruma kwenye uwanja wa Orlando kuanzia saa mbili na nusu usiku.
Uwanja wa Orlando ni miongoni mwa viwanja vizuri vilivyopo kwenye jiji la Polokwane  moja kati ya miji maarufu nchini humo.
Kocha mkuu wa Bafanabafana Gordon Igesund amefurahishwa na uteuzi wa kiwanja hiko akiamini ni moja kati ya viwanja vizuri kutumika na timu yake ya taifa katika uandaaji wa mechi za kimataifa.
CHIPOLOPOLO HELD UP IN LUSAKA
Timu ya taifa ya Zambia wanachipolopolo usiku wa kuamkia leo ilishindwa kukwea pipa kuelekea nchini Ghana kutokana na kuchelewa kukamilisha taratibu za safari hiyo.
Shirikisho la soka la Zambia limethibitisha timu yao kuwekewa vikwazo Afrika kusini ambako waliweka kambi kujiandaa na mchezo huo wa hapo kesho katika dimba la Kumasi dhidi ya wenyeji wao Ghana The Black stars.
Mpaka tunaingia mitamboni kikosi hicho bado hakijapewa kibali ya kusafiri kutoka bondeni Afrika kusini kuelekea nchini Ghana, hata hivyo Shirikisho la Zambia limeahidi kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha suala hilo linamalizika usiku huu.
Msafara wa Zambia umejumuisha makipa watatu, mabeki saba, viungo tisa na washambuliaji watano.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni