Kisiwa cha Saanane kimetangazwa rasmi
kuwa Hifadhi ya Taifa kufuatia Tangazola Serikali Namba 227 lililotolewa hivi
karibuni.Kutangazwa kwa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Saanane kunafuatia
kupitishwakwa Azimio la Bunge mwezi Oktoba mwaka jana lililoridhia kupandishwa
hadhikwa kisiwa hicho kutoka Pori la Akiba na kuwa Hifadhi ya Taifa.
Hifadhi ya
Taifa ya Kisiwa cha Saanane itakuwa na ukubwa wa kilomita za mraba2.18 na
itajumuisha maeneo ya lililokuwa Pori la Akiba , Visiwa vya Chankendekubwa na ndogo pamoja na eneo la maji ya Ziwa
Victoria linalozunguka visiwahivyo.
Kuanzishwa
kwa Hifadhi mpya ya Taifa ya Saanane kutawezesha haja yakuongeza spishi
mbalimbali za wanyamapori na hivyo kuongeza utalii wa mjini,utalii wa ndani, utafiti na kutoa elimu kwa
vitendo kwa wanafunzi na wananchiwatakaotembelea hifadhi hii mpya.Aidha, uamuzi huu utasaidia kutunza hali ya
bioanuwai, uhifadhi wa mazalia namakuzio ya samaki na uendelezaji wa
utalii wa mjini kuendelea kuimarika.
Kabla ya kupandishwa hadhi, Kisiwa cha
Saanane kilikuwa Bustani ya wanyamamwaka
1964 kabla ya kupandishwa hadhi kuwa Pori la Akiba mwaka 1991.Ilipofika
mwaka 2006, Serikali ilikikabidhi kisiwa hicho kwa Shirika la Hifadhi zaTaifa kwa ajili ya kukiendesha na kusimamia
mchakato wa kukipandisha hadhikuwa Hifadhi ya Taifa.Kufuatia uamuzi huu, Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA)
sasa litakuwa na jumla ya Hifadhi 16 nchi nzima
ambazo nyingine ni pamoja na Serengeti; ZiwaManyara; Tarangire na Arusha.
Nyingine ni pamoja na Kilimanjaro; Mkomazi;
Saadani; Mikumi; Milima yaUdzungwa; Ruaha;
Kitulo; Katavi; Gombe; Milima ya Mahale na Kisiwa chaRubondo.
Wakati huohuo,
eneo la Hifadhi ya Taifa Gombe limeongezwa ukubwa
kutokaKilometa za mraba 33.74 hadi kufikia
kilometa za mraba 56. Uamuzi huuunatokana na Tangazo la Serikali Namba
228 lililotolewa hivi karibuni ambalolinafuatia Azimio la Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania lililotolewamwaka jana linalohusu kuridhiwa kwa uamuzi wa
kurekebisha mipaka ya Hifadhiya Taifa Gombe
kwa kuondoa eneo la makaburi na kuliacha kwa wananchi pamoja na
kujumuisha eneo la ufukwe wa maji ya Ziwa Victoria na eneo laukanda wa maji.
Kuongezeka
kwa eneo la ufukwe wa ziwa na ukanda wa maji kwenye eneo lahifadhi kutaongeza
wigo wa shughuli za utalii katika Hifadhi kama vile kuogelea,utalii wa boti,
mitumbwi na uvuvi wa kitalii.
Imetolewa na Idara ya UhusianoHifadhi za Taifa
TanzaniaS. L. P 3134ARUSHA
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni