Ijumaa, 6 Septemba 2013

HIFADHI ZA TAIFA TANZANIATAARIFA KWA UMMA



USAHIHI WA TAARIFA ZA MGENI ALIYEUWAWA NA TEMBO NJEYA HIFADHI YA TARANGIRE



Baadhi ya vyombo vya habari nchini jana na leo vimekuwa vikiripoti juuya tukio la kuuwawa na tembo kwa mgeni kutoka Marekanianayefahamika kama Thomas Vardon Macfee (58) tarehe 31.08.2013 katikaHifadhi ya Taifa Tarangire.

Shirika la Hifadhi za Taifa linapenda kuweka usahihi wa taarifazilizoripotiwa kama ifutavyo:-Tukio la mgeni husika lilitokea nje ya Hifadhi ya Tarangire katika kijiji chaKakoi kambi ya Tarangire River Camp, wakiwa wanafanya utalii wakutembea kwa miguu “Walking Safari”. 

Baada ya kuvamiwa nakuumizwa, mgeni huyu alifikishwa katika zahanati ya Hifadhi yaTarangire na watumishi wa kambi aliyofikia iliyo nje ya hifadhi kwa ajiliya matibabu ya huduma ya kwanza na alipofikishwa, alifariki dunia.Hivyo basi, Shirika linapenda kusahihisha kuwa
tukio lililopelekea kifocha mgeni lilitokea nje ya Hifadhi ya Tarangire na si ndani kamailivyoripotiwa.

IMETOLEWA NA 

IDARA YA UHUSIANO

HIFADHI ZA TAIFA
S.L.P 3134ARUSHA
05/09/2013
 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni