![]() |
Kulia ni Boniface Wambura afisa habari wa TFF, katikati ni Angetile Osiah katibu mkuu TFF, na wa mwisho kushoto ni Jackson Mbando meneja uhusiano wa Airtel |
Timu ya taifa ya Airtel rising stars ya Tanzania,
leo imekabidhiwa bendera tayari kwa ajili ya safari ya kuelekea nchini Nigeria
kushiriki mashindano ya dunia ya Airtel rising stars yatakayotimuvua vumbi
September 16 mwaka huu.
Timu hiyo inayoundwa na wachezaji 32 waliopatikana
kwenye kombaini za mikoa, 16 wakiwa ni wavulana na 16 wasichana wanataraji
kuondoka kesho wakiwa na kauli mbiu ya kurejea nchini na ubingwa wenye thamani
ya kitita Dola 10,000/= sawa na zaidi ya Millioni 16 kwa pesa ya Tanzania.
![]() |
Katibu mkuu wa TFF Angetile Osiah akinena jambo |
Meneja uhusiano wa kampuni ya simu za mkononi ya
Airtel ambao ndiyo wadhamini wakuuwa michuano hiyo Jackson Mbando amewataka
wachezaji kuwa na uelewa juu ya kile wanachokwenda kukifanya kwakuwa haya ni
mashindano makubwa ya dunia na jukumu lao kubwa ni kuhakikisha wanarejea
nyumbani na ushindi.
“Mashindano ya Airtel rising stars ni mashindano
makubwa nandiyo maana yamepewa heshima kubwa sana na shirikisho la soka nchini
TFF, hii ni nafasi ya kwenda iwakilisha Tanzania na mtakuwa mabalozi wazuri
haya si mashindano ya chandimu haya ni mashindano makubwa ya dunia.”
![]() |
Wambura akitafakari jambo |
Akizungumza wakati wa kukabidhi bendera ya Tanzania
kwa manahodha wa timu hizo mbili, katibu mkuu wa shirikisho la mpira wa miguu
nchini TFF Angetile Osiah amewataka vijana kuwa wasikivu na kufata maelekezo
wanayopewa na walimu wao ili kuondokana na lawama endapo timu itashindwa
kufanya vizuri.
“leo mnabeba jukumu la ubalozi ni jukumu zito sana,
unapokuwa balozi unatakiwa ubebe sifa zinazolingana na unachokwenda kushiriki”
“Tuna jukumu zito sana la kubeba hiyo dhamana,
kwahiyo tuhakikishe kila tunachoenda kukifanya ni lazima ujiulize hiki ndicho
nilichoambiwa kukifanya?”
"Nidhamu binafsi nidhamu ya ufundi na je mwalimu
amekuambiaje, kufuata maelekezo ya mwalimu ni kitu muhimu sana”.
![]() | |
Timu ya Airtel rising stars ya wasichana ikikabidhiwa bendera ya Taifa |
![]() |
Timu ya Airtel rising stars ya wavulana ikikabidhiwa bendera |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni