Kiungo Jamal Mohammed na mshambuliaji Dennis Oliech
wanaokipigia soka nje ya Kenya, tayari wameshaungana na kikosi cha timu ya
taifa ya Kenya The Harambee stars kitakachojitupa dimbani jumapili kukipiga
dhidi ya Namibia katika mchezo wa mchujo wa kombe la dunia 2014.
Katika mazoezi ya jioni ya leo wachezaji 22 kati ya
27 ndiyo walioripoti wakati wengine watano wanategemewa wakati wowote kutoka
sasa kujiunga na kikosi cha The Harambee.
Kocha msaidizi wa Kenya James Nandwa amesema kuwa
matokeo ya mechi hiyo muhimu yatawawezesha kupata mterekemko katika michuano
mingine ya FIFA pamoja na kuipandisha timu hiyo katika viwango vya ubora vya
soka duniani.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni