Jumatatu, 23 Septemba 2013

DIMBANI AFRIKA



0-0 DRAW PUTS HOLDERS AHLY AND PIRATES INTO SEMI-FINALS
Mabingwa watetezi wa ligi ya mabingwa barani Afrika Al Ahly pamoja na Orlando Pirates wamefanikiwa kutinga kwenye hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo baada ya kutoka sare ya kutofungana mjini Soweto usiku wa kuamkia leo.
Al Ahly ktoka nchini Misri imemaliza kileleni mwa kundi A ikiwa na alama 11 na timu hiyo itapapatuana na Coton Sport ya Cameroon kwenye nusu fainali mwezi ujao kwa maana ya Octoba mwaka huu.
Nao Orlando Pirates ya bondeni Afrika kusini watakwaana na Esperance ya Tunisia katika hatua hiyo ya nusu fainali.
Hata hivyo katika mchezo huo wa hapo jana pia ulitoa nafasi kwa wawakilishi wa Congo Ac Leopards kufuzu nusu fainali kabla ya kikosi hicho kukubali kichapo cha mabo 4-1 toka kwa Zamalek katika mechezo uliopigwa El Guna nchini Misri.
Leopards na Zamalek zote zimemaliza zikiwa na alama 7, alama moja nyuma ya Orlando Pirates ambao wamefanikiwa kusonga katika hatua hiyo wakiwania kuvuka daraja la kutinga kwenye fainali ya champions league Afrika.
TAARIFA NYINGINE TOKEA NCHINI MISRI
Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Misri Mmarekani Bob Brdaley ametangaza majina ya wachezaji 10 wanaokipigia nje Misri kwaajili ya mechi zao cha mchujo hatua ya mtoano kombe la dunia 2014.
Kocha huyo anataraji kutangaza kikosi kamili hivi karibuni atakachokitumia wakati wa mechi yao dhidi ya Ghana The Black Stars itakayopigwa katika dimba la Baba Yara mjini Kumasi Octoba 15 pamoja na ile ya marudiano watakayokuwa nyumbani nchini Misri mwezi mmoja baadae.
Wachezaji hao ni Mohammed Gedo, Ahmed El-Mohammed, Hossam Ghaly, Mahmoud Kahraba na Ibrahim Salah.
Wengine ni Mohammed Salah, Mohammed El-Neny, Al-Salmiya, Amri Zaki na Adam El-Abd.


GABON SACK COACH PAULO DUARTE
Shirikisho la mpira wa miguu la Gabon limemtimua kocha mkuu wa timu ya taifa ya Gabon Paulo Duarte kufuati kikosi hicho kuondolewa kwenye kampein ya kuwania kutinga fainali za kombe la dunia mwakani zitakazopigwa nchini Brazil.
Katika taarifa iliyotolewa na shirikisho hilo mapema hii leo inaeleza kuwa kocha huyo ataendelea kubaki kwenye shirikisho akiwa kama mkurugenzi wa ufundi.
Kocha huyo aliteuliwa kukinoa kikosi cha Gabon mwezi April mwaka jana kwa mkataba wa miaka miwili, mkataba ambao ulitaraji kumalizika mwezi April mwakani hata hivyo tayari shirikisho limeuvunja mkataba huyo baada ya kuonekana hana msaada wowote katika kikosi hicho.
Kocha huyo mwenye miaka 44 mbali na kushindwa kuipeleka Gabon kwenye fainali ya kombe la dunia mwakani pia ameshindwa kuiwezesha timu hiyo kucheza fainali za CHAN zitakozounguruma mapema mwakani bondeni Afrika ya kusini.
SENEGAL STILL TO DECIDE ON VENUE FOR WORLD CUP PLAY-OFF
 Shirikisho la soka la Senegal limeshindwa kutekelezwa agizo la shirikisho la soka duniani FIFA lililowataka kukamilisha taarifa sahihi za lini na wapi watacheza mchezo wao wa marudiano hatua ya mtoano dhidi ya Ivory Coast.
Rais wa shirikisho hilo Augustin Seghor amesema kuwa wanataraji kukutana leo na kesho kujadili juu yaagizo hilo huku wakiwa na pendekezo la nchi mbili ambazo ni Gine na Morocco, moja kati ya nchi hiyo itatumika kuandaa mtanange huo.
FIFA ilitoa agizo kwa timu zote kumi ambazo zitachuana kwenye hatua ya mtoano kupelekeza taarifa rasmi za siku husika pamoja na viwanja vitakavyotumika kucheza mechi zao za mchujo wa kombe la dunia ambazo za awali zinataraji kupigwa kati ya Octoba 11 hadi 15 wakati zile za marudiano zitapigwa November 15 hadi 19 mwaka huu.
Nchi zingine ambazo pia zinakibarua kizito cha kuwania nafasi 5 za uwakilishi wa bara la Afrika kwenye kombe la dunia mwakani nchini Brazil ni Ivory Coast, Ethiopia, Ghana, Misri, Tunisia, Algeria, Burkinafaso, Cameroon na Nigeria.
RWANDA: KIGALI MTN HALF-MARATHON SET FOR OCTOBER 20
Shirikisho la riadha la Rwanda limearifu kuwa mashindano ya riadha ya m bio fupi maarufu kama Kigali half –marathon kwa mwaka yanataraji kufanyika Octoba 20 katika mji wa Kigali.
Mashindano hayo ya Kilometa 20 kwasasa yanadhaminiwa na kampuni ya MTN na siyo Coca cola kama ilivyokuwa hapo awali na udhamini wa kampuni hiyo sasa utajumuisha matangazo yote ya radio, magazeti pamoja na television.
Katibu mkuu wa shirikisho hilo Johnson Rukundo amesema kuwa shindano hilo litahusisha wanariadha wazawa pekee hata hivyo bado wanajadili ni zawadi zipi zitatolewa kwa watakao ibuka na ushindi.
Ikumbukwe mshindi wa mwaka jana kwa wanaume alikuwa ni Robert Kajuga aliyetumia muda wa dakika 57 na sekunde 12 wakati kwa wanawake alikuwa ni Claudette Mukasakindi aliyetumia saa moja na dakika 9 na sekunde 8.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni