WIN ENSURES QUALIFICATION FOR GHANA
Timu ya
taifa ya Ghana inapewa nafasi kubwa ya kufuzu katika hatua ya mtoano ya kombe
la dunia 2014 endapo wataepuka kupoteza mchezo wa o dhidi ya Zambia September
06 mwaka huu.
Ghana The
Black Stars wanashikilia usukani wa kundi D wakiwa na alama 12 alama moja zaidi
ya Zambia wana Chipolopolo na timu zote mbili zinalia na majeruhi waliopo
vikosini hapo.
Ghana
watamkosa nahodha wao Asamoah Gyan
wakati kocha wa Zambia Herve Renard
ameshauriwa kutafuta plan B kukiwezesha kikosi chake kuwa imara kuelekea kwenye
mtanange huo.
SAINFIET RUES BOTSWANA DEFEAT
Kocha mkuu
wa Malawi Tom Sainfiet amesikitishwa kuona kikosi chake kikipoteza mchezo muhimu wa kujipima nguvu usiku wa kuamkia leo
ambao waliutumia kama maandalizi ya mwisho kuelekea kwenye mchezo wao wa mchujo
wa kombe la dunia.
Malawi
ilikubali kipigo cha goli 1-0 toka kwa Botswana ikiwa ni mchezo wa kimataifa wa
kirafiki kujiandaa kuwakabili mabingwa wa kombe la mataifa Afrika Nigeria The
super Eagles.
Aidha Tom
amezielekeza lawama zake kwa mlinda mlango wa Malawi Charles Swini aliyeonekana kuruhusu goli la wazi lililoiharibia mipango
timu yake, kitendo
ambacho anakitafsiri ni uzembe wa kipa huyo.
Malawi
imeondoka leo nchini Botswana kuelekea Nigeria ambako watashuka dimbani
jumamosi hii kukipiga dhidi ya wenyeji wao The super Eagles wakati Malawi wakihitaji
ushindi katika mchezo huo, wenyewe Nigeria sare tu inawatosha.
Wakati huo
huo kikosi cha Nigeria leo kimefanya mazoezi katika uwanja wa UJ ESENE, uwanja ambao utatumika kuandaa mtanange
huo.
MICHO LOOKS TO NEMESIS FOR INSPIRATION
Kocha wa
kikosi cha Uganda The Cranes Milutin
Sirijiovich Micho amewataka mashabiki wa soka kutokitabiria mabaya kikosi chake kuelekea kwenye mchezo wao wa
kuisaka tiketi ya kutinga fainali za kombe la dunia mwakani dhidi ya Senegal.
Uganda
watamenyana na Senegal wikiend hii Marakesh nchini Morocco, na hisia
za mashabiki wengi wa soka barani Afrika wanauzungumzia mchezo huo utakuwa ni
mwisho wa safar ya Uganda katika michuano hiyo
wakati ikiwa ni tiketi kwa Senegal kufuzu katika
hatua ya tatu ya mtoano.
Mchezo wa
awali kati ya wawili hao uliopigwa Kampala nchini Uganda
ulimalizika kwa sare ya mabao moja moja, na timu
hizo zinachuana vikali wakitofautiana kwa alama moja.
NCHINI
KENYA
Nahodha wa timu ya Taifa ya Kenya The Harambee stars
Victor Wanyama ameungana na kikosi
hicho kilichopo kambini kikijiwinda dhidi ya Namibia katika mchezo wa
kukamilisha ratiba ya mchujo ya kombe la dunia mwakani nchini Brazil.
Wanyama anaungana na wachezaji wengine wa kimataifa Denis Oliech na Jamal Mohammed ambao tayari wamesharipoti mapema
hapo jana.
Kocha msaidizi wa Kenya amesema kuwa kikosi chake
kinaendela na mazoezi kujiimarisha kuelekea katika mchezo huo wa kundi F.
FOUR PLAYERS AT WARRIORS TRAINING
Wakati vikosi vingine vikionekana kuwa na ari
kuelekea kwenye mechi zao za mchujo, huko Zimbabwe kocha mkuu wa timu taifa ya
nchini humo Ian Gorowa ameshangazwa
kuona kikosi hicho kikishindwa kufanya mazoezi jana na leo
kutokana na asilimia kubwa ya wachezaji wake kushindwa kuripoti
katika kikosi hicho.
Taarifa za ndani zinasema kuwa ni wachezaji wanne
pekee ndiyo walioripoti hapo jana wakati hata viongozi wenzake wa benchi la
ufundi akiwemo kocha msaidizi nao wameshindwa kujiunga na kikosi hicho
kilichoingia kambini kujiandaa kuikabili Msumbiji
wikiend hii.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni