Jumanne, 3 Septemba 2013

PAN AFRICAN YAGOMEA UCHAGUZI MKUU YAITISHA MKUTANO WA WANACHAMA



 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Sisi wanachama wa timu ya PAN AFRICAN FC tunasema hatuko tayari kufanya uchaguzi bila ya kufanyika mkutano mkuu.


Mkutano mkuu ni haki yetu kwa mujibu wa katiba Ibara ya 20, jambo linalo sikitisha viongozi tuliowapa dhamana ya kuongoza klabu yetu katika uchaguzi wa tarehe 18/04/2009 mpaka wanamaliza muda wao tarehe 18/04/2013 miaka mine kwa mujibu wa katiba ibara ya 29:1 hawajaitisha mkutano mkuu hata mmoja hivyo kutunyima fursa ya kuchangia maendeleo ya timu yetu.

Mpaka hivi sasa hatujui mapato na matumizi ingawa viongozi hao wanachukua kodi ya jingo letu,hatujui pesa hizo zinatumika kwa matumizi gani na timu hatuna hatushiriki mashindano yoyote.
Cha kushangaza na kustaajabisha viongozi hao wameshikilia kutaka uchaguzi na hawataki kusikia suala la mkutano mkuu na wanaungwa mkonon na baadhi ya viongozi wa IDFA.

Sisi tunasema hatuwezi kwenda kinyume na katiba yetu tunachowaomba viongozi wa IDFA, DRFA na TFF watuelewe sisi tunataka sana uchaguzi lakini kwanza tufanye mkutano mkuu tujue kazi za kamati ya utendaji kwa muda wa miaka mine waliyokaa madarakani tupatiwe mahesabu, mapato na matumizi yaliyokaguliwa na mkaguzi anayetambuliwa kisheria kwa mujibu wa katiba yetu, kwa kipindi chote walichokaa madarakani kinyume na hivyo hatupo tayari kufanya uchaguzi na ikibidi tutaenda mahakamani kudai haki yetu ya kikatiba.


Hivyo wasije kutuelewa viabaya tunataka uma wapenda soka wote watuelewe, haki tunayodai na kuitaka.
Mwisho tunatoa taarifa kwa wanachama wote wa PAN AFRICAN FC waliolipia kadi zao na wote wasiolipia kadi zao wafike katika mkutano utakaofanyika siku ya jumamosi tarehe 07/09/2013 shule ya msingi mnazi mmoja saa 4:00 asubuhi kila mwanachama atakaepata taarifa hii amuarife mwenziwe.
Taarifa imetolewa na
MZEE ALLY ABBASY
MWANACHAMA NO.0059
KWA NIABA YA WANACHAMA WOTE
0755980840.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni