Jumatatu, 2 Septemba 2013

KPL STOOOOOP, THE HARAMBEE STARS VS NAMIBIA GO ON



Ligi kuu nchini Kenya KPL itasimama kwa muda wikiend hii kupisha mchezo wa kimataifa kati ya wenyeji Kenya The Harambee stars dhidi ya Namibia.



Kenya itashuka dimbani jumapili hii September 08 kuikabili Namibia, katika mchezo wa kuwania nafasi ya kutinga kwenye fainali za kombe la dunia mwakani nchini Brazil.


Shirikisho la mpira wa miguu la Kenya limesema kuwa mwishoni mwa wiki hii watakuwa na kibarua kizito kuisaidia timu yao kuibuka kidedea katika mchezo huo, ndiyo maana wamelazimika kusimamisha mechi zote za ligi zilizopaswa kupigwa kuanzia ijumaa hadi jumapili.


Moja kati ya mechi iliyopangwa kucheza wikiendi hii ni pamoja na ile ya Ulinzi stars dhidi ya Sony Sugar na inaelezwa kuwa beki tegemezi wa Ulinzi stars Mohammed Hassan ni miongoni mwa wachezaji 27 wanaounda kikosi cha The Harambee stars chini ya kocha Adel Amrouche



 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni