Jumatano, 18 Septemba 2013

SOKA BARANI AFRIKA


Siku moja baada ya kutimuliwa kwenye benchi la ufundi la AFC Leopards, mbelgiji Luc Emayl ameibuka na kutupa kijembe kwenye uongozi wa klabu hiyo kuwa tayari ameshapata dau nono zaidi katika klabu moja inayofanya vizuri barani Afrika.
Hapo jana Kamati tendaji ya AFC Leopards ilimtimua Mbelgiji huyo aliyekuwa akikinoa kikosi hicho pamoja na wasaidizi wake wa benchi la ufundi kwa kile kinachodaiwa walishindwa kuipa matokeo mazuri timu hiyo.
Pamoja na mambo mengine kocha huyo amesema hana kinyongo kwa maamuzi yaliyofikiwa kwakuwa tayari ameshapata timu mbadala ambayo pia amesita kuiweka hadharani ni timu gani.
Katika hatua nyingine kocha mpya wa AFC Leopards James Nandwa tayari ameanza kibarua chake rasmi hii leo, huku akiahidi kuisaidia timu hiyo kwa hali na mali kuhakikisha kinafanya vizuri kufikia malengo yake iliyojiwekea.
Nandwa ambaye pia ni kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Kenya The Harambee stars alitangazwa hapo jana kubeba mikoba ya mbelgiji huyo akisaidiwa na Mickey Weche kuelekea mwishoni mwa msimu huu wa ligi.
WAKATI HUO HUO
Timu ya taifa ya wanawake ya mpira wa kikapu nchini Kenya imeondoka leo kuelekea Maputo nchini Msumbiji kwaajili ya kushiriki michuano ya ubingwa wa mpira wa kikabu inayotaraji kuunguruma kuanzia September 20 hadi September 29 mwaka huu.
Kenya wamepangwa kwenye kundi B wakiwa sambamba na timu kutoka Angola, Mali, Cameroon, Cape Verde na Nigeria wakati kundi A linajumuisha timu kutoka Senegal, Ivory Coast, Misri, Zimbabwe na wenyeji Msumbiji.
Kenya itaanza kampeni yake ijumaa hii dhidi ya Cameroon wakati mmoja wa wachezaji wanaounda kikosi hicho Samba Mjomba amesema kuwa kikosi chake kipo tayari kimejiandaa vya kutosha wanachohitaji ni kujitupa kwa biii ili kurejea nyumbani na ushindi.


ETO’O WILL BE INVITED FOR KNOCKOUTS
Kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Cameroon Martin Ndtoungou amesisitiza kuwa mshambuliaji mpya wa Chelsea Samuel Etoo ataendelea kubaki kuwa nahodha na chaguo la kwanza la kikosi hicho.
Etoo alitangaza kustaafu kuitumikia timu yake ya taifa saa chache baada ya kumalizika kwa mchezo wao dhidi ya Libya juma lililopita.
Kocha huyo amesema kuwabado wanamtambua kuwa Etoo ni nahodha wa timu yao kwakuwa hajavunja mkataba wa kuitumikia timu yake ya taifa wala kutuma taarifa rasmi ya kustaafu hivyo hivyo kauli yake itabaki kuwa kauli aliyoitamka mbele ya wachezaji wenzake na wala siyo taarifa kwa shirikisho.
Tayari Cameroon imeonesha nia ya kumuita mshambuliaji huyo wakati wa mechi zake za mtoano mchujo wa kombe la dunia dhidi ya Tunisia mwezi Octoba na mwezi Novemba mwaka huu.
HUKO TUNISIA nahodha wa zamani wa Uholanzi Ruud Krol amekubali kuingia mkataba wa miezi miwili kuinoa kikosi cha timu ya taifa ya Tunisia kuelekea kwenye mechi zake mbili za mchujo wa kombe la dunia 2014.
Taarifa za kocha huyo kusaini mkataba hii leo, zimebainika kupitia mtandao wa shirikisho la mpira wa miguu la Tunisia.
Kocha huyo sasa rasmi kuanza kazi akirithi mikoba ya Nabil Maaloul aliyeamua kujiweka kando na timu hiyo kufuatia kichapo cha magoli 2-0 walichopokea toka kwa Cape Verde katika mchezo wa mwisho wa makundi September 7 mwaka huu.
Ikumbukwe Tunisia imetinga kwenye hatua hiyo ya mwisho ya mchujo kutokana na Baraka za shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA ambalo liliwazawadia timu hiyo alama tatu baada ya kujiridhisha kuwa Cape Verde ilimtumia mchezaji asiye na sifa wakati wa mechi yao hiyo.
FIFA WANTS PLAYOFF DATES BY FRIDAY
Shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA limesisitizia timu zote kumi ambazo zimetingwa kwenye hatua ya mwisho ya mchujo wa kombe la dunia, kuthibitisha tarehe na eneo husika wakatayocheza mechi zao husika hadi kufikia ijumaa ya September 20 mwaka huu.
Timu hizo ni Ivory Coast, Senegal, Ethiopia, Nigeria, Ghana, Misri, Tunisia, Algeria, Burkina Faso na Cameroon.
Mechi za mkondo wa kwanza ambazo zitapigwa nyumbani zimepangwa kati ya Octoba 11 hadi 15 wakati zile za marudiano zimepangwa kati ya Novemba 15 hadi 19 mwaka huu.
Kwa mujibu wa ratiba Ivory coast wataanzia nyumbani dhidi ya Senegal, Ethiopia wakiialika Nigeria, huku Tunisia ikipapatuana na Cameroon.
Mechi zingine Algeria watakuwa wenyeji wa Burkina Faso wakati Ghana watamenyana na Misri.
Hata hivyo tayari Ghana wameshatuma majibu kwa FIFA wakilichagua dimba la Baba Yara lililopo Kumasi pamoja na kuichagua Octoba 13 kuwa ni siku itakayotumika kucheka mchezo huo wa awalia.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni