Jumamosi, 7 Septemba 2013

MICHEZONI



GHANA REACH LAST PHASE OF QUALIFIERS
Timu ya Taifa ya Ghana imefanikiwa kutinga kwenye hatua ya tatu ya mtoano ya kombe la dunia baada ya jana kumtandika Zambia magoli 2-1 katika mchezo wa  mchujo wa kundi D.
Ghana The Black Stars sasa inaungana na Algeria, Misri na Ivory katika hatua hiyo ya tatu ya mtoano ambapo washindi wa jumla wa makundi yote kumi watachuana katika mechi za nyumbani na ugenini ili kuwapata wawakilishi wa bara la Afrika katika michuano ya kombe la dunia itakayounguruma mwakani nchini Brazil.
Ghana ilikuwa ni nchi pekee ya Afrika iliyong’ara kwenye michuano ya kombe la dunia iliyopita, baada ya kufanikiwa kutinga hadi kwenye robo fainali ikiondolewa kishujaa kwa mikwaju ya penalty dhidi ya Uruguay.
DIPELA EXPLAINS CHAN DRAW DECISION
Mwenyekiti wa michuano ya mataifa bingwa barani Afrika CHAN Andrew Dipela ameelezea uamuzi wa kuliteua jiji la Cairo nchini Misri kutumika katika zoezi la upangaji wa ratiba ya CHAN na si Afrika kusini kama wengi walivyodhani hapo awali.
Ikumbukwe Afrika kusini ndiyo wenyeji wa michuano hiyo ambapo itashudiwa timu 16 zikichuana kuwania ubingwa huo pamoja na mambo mengine bado haijawa kigezo cha kamati ya mashindano kuipa heshima ya upangaji wa ratiba nchini hiyo ambayo itafanyika September 18 mwaka huu.
Inasemekana siku mbili kabla ya upangaji wa ratiba hiyo, pia katika jiji hilo kutakuwa na upangaji wa ratiba ya mechi za mtoano za mchujo wa kombe la dunia 2014.
Timu zote 16 zilizofanikiwa kutonga kwenye fainali za CHAN zinataraji mapema mwezi ujao kupigwa msasa kuelekea kwenye michuano hiyo itakayounguruma mwezi January mwakani.
KARUTURI SUSPEND COACH OMONDI
Siku moja baada ya uongozi wa Karuturi sport kumsimamisha kocha mkuu wake James Omondi, kocha huyo umeibuka na kudai hana kinyongo na maamuzi hayo licha ya kushangazwa na hatua hiyo.
Katika barua iliyotumwa kwa shirikisho la soka la Kenya Alhamis ya wiki hii, Uongozi wa Karuturi umetanabahisha kuwa umemsimamisha kocha huyo kutokana na kushindwa kuipa matokeo mazuri timu yao inayoshiriki ligi kuu nchini humo.
James Omondi ambaye ni kocha msaidizi wa zamani wa Thika United alijiunga na kikosi cha Karuturi mapema mwaka huu akirithi mikoba ya Michael Nam aliyeamua kuachana na kibarua hicho ili kujiendeleza kitaaluma.
Toka ajiunge na klabu hiyo ambayo kwasasa inakamata mkia wa ligi nchini Kenya, Omondi ameiweza kushinda michezo miwili, kudraw michezo sita na kufungwa michezo nane, hatua ambayo imewawezesha kutwaa alama 16 pekee, zikiwa ni alama 25 nyuma ya vinara wa ligi hiyo Gor Mahia.
STADIUM DILEMMA CONTINUES FOR EGYPT
Shirikisho la mpira wa miguu la Misri bado liko njia panda likihaha kutafuta kiwanja kitakachotumika kuandaa mchezo wa mchujo wa kombe la dunia kati ya timu ya Taifa ya Misri dhidi ya Gine jumanne ijayo.
Awali shirikisho hilo lilitangaza dimba la Borg Al Arab kuwa mwenyeji wa mtanange huo kabla ya wizara ya mambo ya ndani ya Misri kuzuia kiwanja hicho kuumika kutokana na sababu za kiusalama.
Kocha msaidizi wa Misri Diaa Al Sayed amesema kuwa mpaka sasa bado hawajajuwa ni wapi watacheza mchezo huo, wanasubiri taarifa ya shirikisho la soka nchini humo ambalo limeahidi kutavunja kiwanja mbadala kabla ya kufikia September 10 mwaka huu.
Misri ndiyo vinara wa kundi G wakiongoza kwa alama 15 na tayari imeshafuzu kwenye hatua ya tatu ya mtoano itakayoanza kupigwa mapema mwezi November.
Misri watakuwa wenyeji wa Gine September 10 mwaka huu wakati Algeria ikiwaalika Mali katika mchezo wa kundi H.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni