Siku moja baada ya mabingwa wa ligi kuu Yanga Afrika
kudaiwa kupata katibu mpya, baraza la wazee la Yanga limekanusha kumtambua
katibu huyo na kumtaka aondoke mara moja klabuni hapo.
Katibu huyo mpya Patric Naggi raia wa Kenya inadaiwa
ameletwa kukalia kiti cha kaimu katibu mkuu wa sasa Lawrence Mwalusako bila ya
kutokuwepo taarifa rasmi kutoka katika kamati tendaji ya Yanga chini ya
Mwenyekiti wake Yusuph Mehboob Manji.
Katibu wa baraza hilo la wazee laYanga Ibrahim Omary
Akilimali “Abramohvich” amesema kuwa ujio wa Patric Naggi umekuwa ni wa mashaka
kwasababu si mwanachama wa Yanga na hastahili kushika wadhifa wowote klabuni
hapo kwamujibu wa katiba ya Yanga.
Mzee Akilimali ametaja kuwa ujio wa Patrick Naggi,
kamati tendaji haina taarifa, baraza la wazee hawana taarifa, baraza la
wenyeviti na makatibu wa mikoa pia hawana taarifa na kamati tendaji ilipaswa
ipitishe taarifa ya ujio wa katibu huyo mpya.
Baraza likaenda mbali zaidi na kusema kuwa
hawamtambui katibu huyo na si mwanachama wa yanga hivyo hawataki alete
mgawanyiko miongoni mwa wanachama kwa kuwa ujio wake hauna utofauti na tapeli.
Sababu kubwa za baraza hilo kutoutambua ujio wake ni
kutokana na kutokuwepo taarifa rasmi lakini pia inaelezwa kuwa hakuwa na
mwenyeji wowote. “tunawasiwasi asije kuwa ni tapeli hivyo
hatumtambui, arudi kwa walomleta kama wapo wampe pesa ya kulala na chakula
pamoja na tiketi leo arudi kwao Kenya”
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni