Jumatatu, 2 Septemba 2013

TAIFA STARS KUZITAFUTA ALAMA TATU GAMBIA



Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa stars imeendelea na maandalizi kujiandaa kuelekea kwenye mchezo wao dhidi ya Gambia september 08 mwaka huu nchini Gambia ikiwa ni mchezo wa kukamilisha ratiba ya mchujo ya michuano ya kombe la dunia 2014

Kocha wa Taifa stars inayodhaminiwa na kampuni ya bia ya Kilimanjaro Kim Paulsen leo amefanya mabadiliko mengine katika kikosi hicho, amemtoa Agrey Moris na kumuita kikosini Henry Joseph Shindika


Aidha imeelezwa kuwa ligi kuu imepelekea kikosi cha Stars kukosa mchezo mmoja wa kimataifa kirafiki kujiandaa kuelekea kwenye mchezo wao wa September 08 mwaka huu dhidi ya Gambia
 


Taifa stars inakamata nafasi ya tatu kundi CHE ikiwa na alama 6 ikizidiwa alama 7 na vinara Ivory Coast

Morocco wenyewe wako katika nafasi ya pili wakiwa na alama 8 wakati Gambia wakifunga dimba kwa alama yao 1

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni