Mabingwa wa zamani wa ligi kuu wekundu wa msimbazi
Simba wametoa siku 6 kuanzia hii leo hadi September 09 mwaka huu kwa yoyote
anaehusika na kuuza bidhaa feki za Simba kujisalimisha klabuni hapo ikiwa ni
utekelezaji wa oparesheni mpya ya kamatakamata bidhaa feki zenye nembo ya Simba
Tanzania nzima.
Mwenyekiti wa wadhamini wa Simba Mzee Hamis Kilomoni
amebainisha kuwa oparesheni hii ni non-stop na mpaka sasa cwamefanikiwa
kukamata bidhaa zinazoshukiwa kuwa bandia zenye thamani ya zaidi Shilling
Million 44,195,000/=./
Kutoka jeshi la polisi, Inspector Mohammed mwenye
dhamana ya kuwakamata watakaobainika kujihusisha na vitendo hivyo ameahidi
kulivanjia njuga hilo pamoja na kuwatia kwenye mikono ya sheria kwawote
watakothibitika kuhusika kwa namna moja ama nyingine.
Nae afisa mwandamizi, mawasiliano na mahusiano ya
umma kutoka tume ya ushindani Frank Mdimi ambao wanahusika na uendeshaji wa
oparesheni hiyo ya kushitukiza katika sehemu mbalimbali, akamtilia msisizito namna wanavyopaswa kujisalimisha ili kuokoa mapato ya klabu husika.
SEHEMU YA BIDHAA ZILIZO KAMATWA
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni