Jumamosi, 28 Septemba 2013

MISS PHILIPPINE ATWAA TAJI LA MISS WORLD 2013

Wakati akiveshwa taji la Miss Philippines


MTAZAME KATIKA MUONEKANO TOFAUTI
HISTORIA YAKE KWA UFUPI
Jina lake kamili anaitwa Megan Lynne Young ni chotara wa kimarekani na Philippine, ni muigizaji na pia ni mtangazaji wa kipindi cha Television na ni mjumbe wa ABS-CBN Star Magic.
Amezaliwa February 1990 huko Alexandria, Virginia, United States, na urefu 1.73 M.
Elimu yake kwasasa anaipata kwenye chuo cha De La Salle-College Of Saint Benilde ambako anasomea utengenezaji wa Filamu.
Miss Ghana Nae Katisha Afrika oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee

Jumanne, 24 Septemba 2013

ASHANTI YAAHIDI POINTS 3 HAPO KESHO

Ligi kuu soka ya Tanzania bara inataraji kuunguruma tena hapo kesho kwa kushuhidiwa mchezo mmoja pekee utakaopigwa kwenye uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini Tabora ambapo wenyeji wa Rhino Rangers watawakaribisha wauza mitumba wa Ilala watoto wa jiji Ashanti United.
 Timu zote zinashuka dimbani zikiwa tayari zimeshacheza mechi tano ambazo kwa upande wa wenyeji Rhino rangers zimewawezesha kuvuna points 4 baada ya kutoka sare michezo minne na kupoteza mmoja wakati kwa upande wa Ashanti yenyewe imepoteza michezo minne na kutoka sare mmoja uliowapa alama 1 pekee.
Afisa habari wa Ashanti United Rajab Marijan amesema kuwa kikosi chao kipo imara kuelekea kwenye mchezo huo licha ya kukabiliwa na majeruhi akiwemo mkongwe Said Maulid.
“Kiujumla kimaandalizi tuko vizuro japo tuna matatizo na wachezaji wawili na kwamujibu wa taarifa ya daktari, wachezaji hao hawatocheza kesho”.
“Mechi za mikoani nguvu ingawaje TFF wakae na kuangalia upya kutokana na aina ya viwanja tunavyokutana navyo pamoja na michezo tunayokutana nayo, michezo ya mikoani imejaa fitna na haiangalii usawa”
Marijan ameongezea kuwa bado wananafasi nzuri ya kupata matokeo mazuri katika mechi zake za nyumbani huku akilitaka shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF kutazama upya viwanja mbalimbali vya mikoani ambavyo vinatumika katika ligi licha ya kuwa katika ubora unaotakiwa.
Tumejipanga kuhakikisha tunashinda dhidi ya Rhino na turudi tukashinde mechi za nyumbani, kulingana na matokeo ya ligi timu hazijapishana sana kwahiyo matokeo hayatushtui”.
Kwa upande wa Rhino Rangers yenyewe wamesema kuwa mchezo huo utatumika kuwapa alama tatu muhimu zitazowaweka katika nafasi nzuri kuelekea kwenye mechi zake zingine za mzunguko wa kwanza wa ligi.
Ligi hiyo itaendelea tena September 28, ambapo mabingwa watetezi Yanga Afrika baada ya kupoteza mchezo wake uliopita mbele ya Azam, wanataraji kuzichanga upya karata zao za kutetea ubingwa watakapoikabili Ruvu shooting katika mchezo utakaopigwa uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.
Huko Tanga katika uwanja wa Mkwakwani Mgambo JKT watamenyama na JKT Oljoro, Mbeya City wakiwakaribisha wagosi wa kaya Coastal Union katika uwanja wa Sokoine mjini humo huku Rhino rangers ikitaraji kujitupa tena kiwanja chake cha nyumbani kucheza dhidi ya Kagera sugar.

WAAMUZI 6 WAFUNGIWA




Shirikisho la mpira wa miguu la nchini humo limewafungia waamuzi 6 kuchezesha mechi zozote katika kipindi cha miezi 6 baada ya kubainika waliforj au walidanganya vyeti vyao vya elimu ikiwa ni vielelzo muhimu kwa waamuzi kuwa navyo hususani vikiwa sahihi na siyo vya kutengeneza.
Hata hivyo bado shirikisho hilo halijatoa tamko rasmi kwa wanahabari nchini humo kuhusiana na sakata hilo.
Waamuzi hao ni Uriah Glah (Accra), Daniel Dorgbertor (Sunyani), Amofa Sarkodie (Obuasi) na Augustine Akugre (Bolga)
Uriah Glah


 Six local referees have been suspended for six months by the Ghana FA for providing fake BECE certificates.
The Basic Education Certificate Exams are the first level of school leavers' documentation in Ghana's curricular ladder.
The nine are Uriah Glah (Accra), Daniel Dorgbertor (Sunyani), Amofa Sarkodie (Obuasi) and Augustine Akugre (Bolga).
Others are Alex Akugre (Tamale), Osman Ouagragou (Bolga), Samuel Kyeremeh Yeboah (Berekum) and Prince Tawiah, (Techiman), together with Frederick Bediako (Accra).
They have been charged with impersonation and providing fake documents.
Speaking to the media on Tuesday, retired referee Alex Quartey hinted that the story was true, but said official word from the Ghana FA is awaited.
Though the GFA and RAG have remained tight lipped, Citi Sports checks show that the charges are the reason why the nine refs have been omitted from the list of officials for this Ghana Premier League season.

TIMESOFMONEY YADHAMIRIA KUINGI KATIKA SOKO LA TANZANIA

24/09/2013: KAMPUNI kubwa duniani yenye utaalamu wa kuwezesha uhamisho wa fedha kwa njia ya mtandao (online) ya Timesof Money, imedhamiria kuingia katika soko la Tanzania, kama sehemu ya mpango wake wa upanuzi barani Afrika.
Katika mpango wake huo, kampuni hii yenye makao yake makuu jijini Mumbai nchini India, inatajaria kuzindua mpango/mfumo wa kutuma fedha nchini toka kwa Watanzania walioko nje ya nchi (remittance) kwa njia ya mtandao (Online).  Mfumo huo ambao unatarajiwa kuleta mapinduzi makubwa nchini, utawawezesha Watanzania kupata/kutuma fedha kutoka mahali popote duniani moja kwa moja katika akaunti zao za benki, kadi za malipo ya kabla (pre-paid cards) pamoja na simu zao za mkononi.
“Katika mkakati huo huo wa kijitanua barani Africa, hivi karibuni tumeingia mkataba na Benki ya Diamond Trust nchini Kenya kutoa huduma kwa wateja wake wa mfumo wa ‘NationHela’,” alisema Afisa Mtendaji mkuu wa TimesofMoney, Avijit Nanda.
Kwa mujibu wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania, idadi ya Watanzania wanaoishi na kufanya kazi nchi mbalimbali duniani/ughaibuni (diaspora) inakadiriwa kuwa zaidi ya million mbili. Na kwa mujibu wa ripoti ya Benki ya Dunia, inakadiriwa kuwa Watanzania hao waliingiza nchini kiasi cha shillingi billion 120 (US$ 75million)mwaka jana. Kwa kutumia huduma hii, Watanzania wanaoishi nje ya nchi wataweza kutuma pesa kwa jamaa na marafiki zao nyumbani, hivyo kuondoa usumbufu wa kusimama katika foleni kwa mawakala wa kuhamisha fedha.
"Idadi ya raia wa nchi za Afrika Mashariki na hasa Tanzania wanaoishi nje ya nchi zao inaendelea kuongezeka na hii ina maanisha uhitaji wa kutuma fedha nyumbani (remittance) pia unaongezeka. Ni kwa sababu hii tumeona kuna umuhumi wa kuingia katika soko hili. Tukiwa na teknolojia ya kisasa, tunatoa ahadi ya huduma bora kwa kutumia wataalamu wenye uzoefu mkubwa katika nyanja hii,” alisema Bw Nanda.
Bara la Afrika linakadiriwa kuwa na idadi ya watu zaidi ya million 30 wanaoishi nje ya nchi zao za asili. Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo-- International Fund for Agricultural Development (IFAD), unakadiria kwamba mwaka jana (2012) wahamiaji hao kwa pamoja wamechangia/ wametuma kiasi cha dola za marekani millioni 38.6 katika fedha kutoka nje, kwa familia na jamii zao nyumbani.
Hata hivyo, moja ya kikwazo kikubwa kwa ukuaji wa mtiririko kutuma fedha nyumbani (remittance) katika nchi za Afrika hasa zile zilizopo Kusini mwa jangwa la Sahara, ni gharama kubwa ya kutuma fedha. Wastani wa gharama ya kutuma fedha kwa Afrika ni karibu 12 % ya juu kuliko wastani wa kimataifa wa 8.96 % na karibu mara mbili ya gharama ya kutuma fedha kwa Asia ya Kusini.
"Gharama kubwa za ada zinazotozwa na makampuni na mawakala wa kuhamisha fedha barani Africa, imekuwa ni kikwazo na imeathiri mtiririko wa kuingiza fedha toka nje ya nchi. Mtumiaji wa mwisho ndiye anayeathirika na kubeba mzigo wa gharama/ada kwa kiasi kikubwa. Kwa kupitai mfumo wa mtandao (online-transactions) tunatarajia  inaweza kusaidia kupunguza gharama hizi kwa kiasi kikubwa, jambo ambalo litatao ahueni kubwa kwa mtumiaji wa mwisho,” bosi huyo wa TimesofMoney alisema.

Kuhusu TimesofMoney :
TimesofMoney ni  kampuni inayoongoza duniani kwa kufanya biashara  ya uhamisho wa fedha  kitaalamu. Kampuni hii inisifika kwa kufanya biashara  na wateja mbalimbali wakiwemo wa rejareja na kitaasisi duniani kote.
Ikiwa imeanzishwa mwaka 2000, TimesofMoney, inatoa ufumbuzi  wa mifumo ya malipo kwa wafanyabiashara.
Huduma zinatolewa duniani kote - kuwezesha uhamisho wa fedha watu kwenda kwenye nchi zao za nyumbani na kutoa huduma ya urahisi wa kutumia internet au simu.
Ikiwa na zaidi ya miaka 12 ya uzoefu, TimesofMoney inajivunia mahusiano mazuri na ya nguvu na wateja wake wakiwemo wale wa rejareja, kitaasisi na pia inaheshima na mafanikio makubwa katika sekta ya fedha kwa miaka kadhaa sasa.
Kampuni hii pia inajuvunia kuwa mbia mkubwa (kuwa na hisa kubwa) katika Mtandao wa Kimataifa, na ni kiongozi wa soko katika mfumo wa malipo. Inasimamiwa na timu ya wataalamu wenye uzoefu kutoka benki na historia nzuri ya fedha.
Maelezo zaidi zinapatikana kwenye tovuti ya kampuni www.timesofmoney.com .
Kwa maswali wasiliana na:
Lucy T. Ngongoseke | Tabasamu Public Relations | (Mobile) +255 754 602674 | lucy@tabasamupr.co.tz
Bhavin Shah | TimesofMoney | (Desk) + 91-22-3098 8491 | bhavins@timesofmoney.com
Mike Omuodo | H+K Strategies | (Mobile) + 254-720910146 | Mike.Omuodo@hkstrategies.co.ke