Jumatano, 30 Oktoba 2013

YAYA TOURE NAMED UN AMBASSADOR



Kiungo wa Manchester City na timu ya taifa ya Ivory Coast Yaya Toure ameteuliwa kuwa balozi wa amani wa program ya mazingira ya umoja wa mataifa UNEP makao makuu yake yaliyopo Nairobi nchini Kenya.
Kiungo huyo mwenye miaka 30 ambaye ni mchezaji pekee kutoka barani Afrika aliyopo katika orodha ya wachezaji 23 wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa mwaka ya FIFA anataraji kuungana wa timu ya wanaopinga ujangili wa wanyama hususani tembo.
Yaya Toure baada ya kuteuliwa kwake amewataka wanaAfrika kumuunga mkono na kushirikiana nae kutokomeza ujangili dhidi ya viumbe hao.
Toure amesema kuwa timu yake ya taifa ya Ivory Coast ilipewa jina la tembo wa Ivory Coast kutokana na uzuri wa wanaviumbe hao na nguvu walizonazo na inawezekana ndani ya taifa lake bado kukawa na uhaba wa wanaviumbe hao kutokana na ukatili wa baadhi ya watu wenye nia ya kufurahisha matumbo yao pekee.
Uongozi wa UNEP umemtaka kiungo huyo mahiri barani Afrika kupaza sauti yake, kutumia uwezo wake na jitihada zake kuelimisha jamii kuacha biashara haramu inayokuza ujangili dhidi ya tembo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni