REDD’S ORIGINAL YAZINDUA TAMASHA LA MITINDO KWA VYUO VYA ELIMU YA JUU
(REDD’S UNI – FASHION BASH 2013)
Dar es Salaam,08 OCTOBER 2013:
Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia kinywaji
chake cha Redd’s Original leo
imezindua tamasha la aina yake la mitindo kwa vyuo vya elimu ya juu. Tamasha
hili litakalojulikana kama “Redd’s Uni-Fashion Bash” kwa mwaka huu litaanza
mwezi huu wa Octoba hadi Novemba na kushirikisha vyuo vyote vya elimu ya juu
vilivyo katika mikoa minne ambayo ni Dar Es Salaam, Kilimanjaro, Iringa na
Mwanza.
Kutoka kulia Meneja masoko TBL Fimbo Butallah, kushoto Meneja wa habari na mawasiliano wa TBL Edith Mushi |
Akizungumza katika uzinduzi huo, meneja Masoko wa
Tbl Fimbo Buttalah alisema; “Tamasha hili
la mitindo lina lengo la kuinua vipaji vya wanafunzi wa vyuo katika tasnia ya
mitindo kupitia maonesho yatakayofanywa katika vyuo, ambapo wanafunzi wenye
vipaji vya ubunifu watapata fursa ya kuonesha ubunifu wao wa mitindo. Hii ni
fursa kubwa kwao kujitangaza na kudhihirisha uwezo wao.”
Bwana Fimbo,
pia alielezea utaratibu wote wa kuwapata wabunifu watakaoonesha kazi zao
jukwaani wakati wa matamasha haya ya aina yake kwa kusema; “Uzinduzi huu
utafuatiwa na usajili wa wanafunzi wabunifu na wanamitindo kupitia fomu maalum
zitakazosambazwa vyuoni, kisha majaji watachambua fomu zote zilizowasilishwa na
kupata wabunifu 10 katika kila mkoa watakaokidhi vigezo, ambao watapata fursa
ya kuonesha mavazi yao siku ya tamasha, pia kutakuwa na nafasi 10 kwa wanamitindo
watakaovaa mavazi hayo jukwaani. Majaji wataangalia vigezo na kupata washindi
ambao watapata zawadi toka kwa kinywaji cha Redd’s Original.”
Akizungumzia zawadi kwa washindi, meneja mawasiliano
na Habari wa Tbl Edith Mushi alisema; Zaidi ya kuwapatia jukwaa wabunifu na
wanamitindo hawa ili waweze kuonesha vipaji vyao, Redd’s pia itawapatia zawadi
za pesa washindi watano katika kila mkoa watakaoshika nafasi za juu kama
ifuatavyo;
WABUNIFU
|
|||
MSHINDI WA KWANZA
|
700,000
|
||
MSHINDI WA PILI
|
500,000
|
||
MSHINDI WA TATU
|
300,000
|
||
MSHINDI
WA NNE NA WA TANO
|
100,000
|
KILA MMOJA
|
|
WANAMITINDO
|
|||
MSHINDI WA KWANZA
|
500,000
|
||
MSHINDI WA PILI
|
400,000
|
||
MSHINDI WA TATU
|
300,000
|
||
MSHINDI
WA NNE NA WA TANO
|
100,000
|
KILA MMOJA
|
Tuna imani kubwa kuwa zawadi hizi zitaongeza
chachu kwa wabunifu kujidhatiti katika kuendeleza ubunifu katika tasnia hii ya
mitindo. Lakini pia matamasha haya yatahusisha burudani mbalimbali za kuvutia
na hivyo kuwa sehemu muhimu ya kuwakutanisha wanafunzi wa vyuo na kada
mbalimbali katika kufurahia na kubadilishana mawazo juu ya masuala ya ubunifu
na mitindo.
Kinywaji cha Redd’s Original kimekuwa mstari wa
mbele katika kuendeleza tasnia ya urembo, ubunifu na mitindo hapa nchini.
Kuhusu TBL
Tanzania Breweries Limited (TBL) inatengeneza, kuuza na kusambaza bia,
vinywaji vyenye ladha ya matunda vilivyo na kilevi na vinywaji visivyo na
kilevi hapa Tanzania. TBL pia ndiyo kampuni mama ya Tanzania Distilleries
Limited pamoja na kampuni shiriki ya Mountainside Farms Limited.
Bia zinazotengenezwa na kampuni ya TBL ni pamoja na Safari Lager,
Kilimanjaro Premium Lager, Ndovu Special Malt, Castle Lager, Vinywaji vingine
vinavyotengenezwa na kundi la makampuni ya TBL ni Konyagi Gin, Amarula Cream,
Redd’s Original na Grand Malt.
Kundi la makampuni ya TBL limeorodheshwa kwenye Soko la Hisa la Dar es
Salaam, limeajiri watu wapatao 1,300 na linawakilishwa nchi nzima na viwanda
vinne vya bia, kiwanda kimoja cha kutoneshea, kimoja cha kutengenezea kimea
pamoja na bohari nane za kusambazia bia.
Kuhusu SABMiller
SABMiller plc moja kati ya makampuni makubwa ya bia duniani ikiwa na
mikataba ya kutengeneza na kusambaza bia kwenye nchi zaidi ya 60 katika mabara
matano. Bia zake ni pamoja na zile za kimataifa kama Miller Genuine Draft,
Peroni Nastro Azzurro na Pilsner Urquell vilevile na bia nyingine zinazoongoza
kwenye masoko ya ndani ya nchi mbalimbali. Nje ya Marekani, SABMiller ni moja
ya kati ya makampuni makubwa yanayotengeneza vinywaji vya Coca-Cola duniani.
Hivi karibuni SABMiller plc ilinunua kampuni ya bia ya Foster’s pamoja na
shughuli zake za uzalishaji nchini India.
SABMiller imeorodheshwa kwenye masoko ya hisa ya London na Johannesburg.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni