Jumatano, 30 Oktoba 2013

RAGE AMFUNGIA MILANGO JUMA KASEJA



Toka huna chako hapa ole wako urudi
Mabingwa wa zamani wa ligi kuu wekundu wa msimbazi Simba hawatarajii kumrejesha kikosini aliyekuwa mlinda mlango wao namba moja Juma K Juma(Juma Kaseja)  walitemana nae mwishoni mwa msimu uliopita.
Mwenyekiti wa wekundu hao Ismail Aden Rage amesema kuwa suala la Kaseja litabaki kuwa historian a wala hawafikirii kumrejesha tena kipa huyo kwakuwa tayari wanae kipa chaguo lao Mganda Abel Dhaira.
Rage amesema kuwa maneno yanayozungumzwa na kuandikwa kwenye baadhi ya vyombo vya habari kuwa Kaseja atarudi Simba ni ya uchochezi na yana lenga kuwavuruga tu.
Dah jamani hamnionei hata huruma?
“Hii habari ya Kaseja karudi Simba inawasaidia nini wanasimba?tuko kwenye premier League ni kutaka kuwavuruga wanasimba waache kuconcentrate kwenye mambo yao, dirisha dogo bado, usajili bado aliyekwambieni tunabadilisha golikipa nani.”
Hakatiw mtu hapa
Tuandike vitu ambavyo vinatusaidia kuleta maendeleo, kila siku mnaandika habari za uwongo yanga kafanya hivi simba kafanya hivi”.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni