Jumatano, 30 Oktoba 2013

ERNIE BRANDS AWAPOZA MASHABIKI WA DAR YOUNG AFRICANS



Jamani tulieni waacheni vijana wangu
Kocha mkuu wa mabingwa watetezi wa ligi kuu soka ya Tanzania bara Yanga Afrika Ernie Brands amewatuliza mashabiki wa Yanga na kuwataka kuacha kuwashutumu baadhi ya wachezaji kuwa wanatumiwa kwa namna moja ama nyingine kuihujumu timu hiyo.
Kauli ya Brands imekuja baada ya  kusikitishwa na kauli za baadhi ya mashabiki wa Yanga waliojitokeza jana uwanja wa Taifa Dar es Salaam wakati wa mchezo wao uliomalizika kwa Yanga kuondoka na alama 3 baada ya kuwabanjua Mgambo JKT magoli 3-0.
Baadhi ya mashabiki wa Yanga walionekana kuendelea kumlaumu mlinda mlango namba moja wa Yanga Ally Mustapha Mtinge Barthez pamoja na nahodha wao Nadir Haroub Ally Canavaro kwa kile wanachokidai walipokea mpunga na kusababisha kutoka sare na watani wao wa jadi wekundu wa msimbazi Simba.
 Brands amesema kuwa hayo yote ni matokeo ya mchezo na wala mashabiki hawapaswi kumlaumu mtu yoyote na badala yake waunge mkono juhudi zinazofanywa na wachezaji wao za kuhakikisha wanatetea ubingwa msimu huu wa ligi.
 They have to support us and not blaming goalkeeper, if someone made a mistake they have to help us and support us in good times and bad times”
 Nae Dakatari mkuu wa Yanga Afrika Nassor Ally Matuzya akafunguka kuhusiana na majeruhi waliopo kikosini hapo na endapo kutakuwa na uwezekano wa kuwa na kikosi chote kamili kuelekea katika mchezo huo dhidi ya JKT Ruvu.
“Kikosi kinaendelea vizuri, tuna majeruhi wachache akiwemo Nizar Khalfani ana majeruhi ya paja kwa nyuma, yupo David Luhende ambaye pia nae anasumbuliwa na paja, Nizar aliumia mazoezini wakati Luhende aliumia wakati wa mechi iliyopita dhidi ya Rhino Rangers”.
“Tunae pia majeruhi Juma Abdul ambaye aliumia mechi iliyopita pamoja na Abdallah Mghui Messi timu inaendelea vizuri na wengine wote wanaendelea na maandalizi”.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni