Alhamisi, 10 Oktoba 2013

HAILE GEBRE SELLASSIE ALIKWA UHURU MARATHON




MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sadick Mecky Sadick ameziomba taasisi, kampuni na idara mbalimbali kujitokeza kudhamini mbio za Uhuru Marathon zinazotarajiw akufanyika jijini Dar es Salaam Desemba 8, mwaka huu.
Mbali na hilo waandaaji pia wametuma mwaliko kwa wanariadha mbalimbali maarufu duniania akiwemo Haile Gebre sellasie ili kumuomba ashiriki mbio hizo.
Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mbio hizo, Sadick alisema, mbali na mialiko waliyotoa lakini mbio hizo ni muhimu zaidi kwaWatanzania kwasasa kwani zina lengo la kudumisha amani, umoja na mshikamano uliopo miongoni mwetu.
Kiongozi huyo ambaye ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi alisema, katika kipindi hiki ambacho kuna baadhi ya watu wanataka kuvuruga amani, umoja na mshikamano miongoni mwa wa Watanzania.
“Katika kipind hiki ambacho kuna baadhi ya watu wanafanya hila za aina mbalimbali ili kutuvuruga ni vyema Watanzania wakazienzi mbio hizi ambazo zimekuja katika wakati muafaka wa kudumisha yale yaliyoasisiwa na waasisi wa taifa hili.
“Hivyo katika kipindi hiki ambacho tunatakiwa tudumishe amani, umoja na mshikamano miongoni mwetu ni bora zaidi tukaona umuhimu wa mbio hizi.
“Ni vyema pia nichukue nafasi hii kuzitaka kampuni, taasisi na watu mbalimbali kuzidhamini mbio hizi ambazo ni zetu sote na zenye umuhimu mkubwa kwa ustawi wa Taifa letu,” alisema Sadick.
Alifafanua kuwa, pale ambapo amani, umoja na mshikamano unapokosekana miongoni mwa  Taifa hakuna hata mmoja atakayesalimika, hivyo ni jukumu la Watanzania wote kuitetea na kuilinda kwa nguvu.
Alisema anajivunia Mkoa wa Dar es Salaam kuandaa mbio hizo kwani jiji hilo lina umuhimu mkubwa wa kutangaza amani iliyopo ndani ya Tanzania.
Kuhusu mbio alisema, kutakuwa na mbio ndefu za kilomita 42, kilomita 21 na kuna zile za kilomita 5 ambazo zitawahusisha watu wa kada mbalimbali, wakiwemo mawaziri, wabunge, wanasiasa na za kilomita tatu zitakazo wahusu zaidi viongozi wa ngazi za juu wa Serikali.
Katibu wa Kamati ya Maandalizi ya Uhuru Marathon, Innocent Melleck alisema, wamealika wanariadha mbalimbali maarufu akiwemo Haile Gebreselassie wa Ethiopia na wana imani kubwa anaweza kushiriki kama mambo yataenda kama yalivyopangwa.
“Tumealika wanariadha mbalimbali maarufu na kama mipango ikienda sawa tumemuomba pia mwanariadha maarufu duniani Haile Gebresellasie kuja kushiriki katika mbio hizo,” alisema.
Mkurugenzi wa Michezo msaidi katikaWizara ya Habari, Utamaduni, Vijanana Michezo, Juliana Yassoda alisema, anaimani kubwa mbio hizo pia zitakuwa chachu kubwa ya kuinua mchezo huo hapa nchini.
“Sio kwa riadha  tu, kuna michezo mingi hapa nchini, lakini ni vyema vyama vya michezo hapa nchini vikaweka mikakati na yotekelezeka ilikuhakikisha Tanzania inafanya vyema zaidi,” alisema.
Mbioza Uhuru Marathon zinatarajiwa kufanyika kilaDesemba 8 ya kila mwaka hapa nchini.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni