JAMHURI
YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI
JESHI LA POLISI TANZANIA
PRESS RELEASE
19/10/2013
JESHI LA POLISI KANDA MAALUM DSM
LINAENDELEA NA MSAKO MKALI NA KUFANIKIWA KUKAMATA WATUHUMIWA 119 KWA MAKOSA
MBALIMBALI.
·
KUKAMATWA
WATUHUMIWA WAWILI WANAOMWAGIA WATU KEMIKALI AINA YA TINDIKALI
·
KUPATIKANA KWA
SILAHA MBILI RIFFLE MOJA, BASTOLA MOJA, RISASI
TATU NA MTUHUMIWA MMOJA
·
KUKAMATWA KWA MAJAMBAZI WATATU
AKIWEMO MWANAMKE WANAOKABA NA KUPORA PIKIPIKI
·
KUKAMATWA KWA WAHAMIAJI
HARAMU KUMI NA SABA WA SOMALIA NA ETHIOPIA
·
KUKAMATWA KWA
MATAPELI WATATU MMOJA AKIWA NA KITAMBULISHO BANDIA CHA IDARA YA USALAMA WA
TAIFA
·
KUKAMATWA KWA
WATUHUMIWA (91), BHANGI, KETE (183),
PULI (34), MISOKOTO (107) NA GONGO LITA (91)
·
RAI MMOJA RAIA WA
SOMALI AKAMATWA NA NYARAKA ZA SERIKALI
·
POLISI KUIMARISHA
ULINZI MKALI WAKATI WA MECHI YA LIGI KUU YA
VODACOM KATI YA SIMBA NA
YANGA UTAKAOFANYIKA TAREHE 20/10/2013
KUKAMATWA WATUHUMIWA WAWILI WANAOMWAGIA WATU
KEMIKALI AINA YA TINDIKALI.
Jeshi la
Polisi Kanda Maalum Dsm, mnamo tarehe
10/10/2013 majira ya saa mbili asubuhi huko maeneo ya Lumumba kariakoo
lilifanikiwa kuwakamata watuhumiwa wawili wanaomwagia watu kemikali aina ya
tindikali, ufuatiliaji huo ulifanywa kwa njia ya mtandao(Electronic
Intelligence Analysis) na kuweza kuwabaini watuhumiwa hao.
katika siku za hivi karibuni kumeibuka tabia
ya matukio ya watu kumwagiwa kemikali aina ya tindikali DSM, Zanzibar na
Arusha. Aidha watuhumiwa hao katika mahojiano ya awali walikiri kuhusika na
tukio moja la kummwagia tindikali mfanyabiashara raia wa LEBANON aitwaye ALLY
S/O IBRAHIMU FARHAT (33) Mkazi wa Upanga tukio ambalo liliripotiwa kituo cha
Polisi Msimbazi MS/IR/7917/2012.
Aidha taarifa
za kiintelijensia zinaonyesha mbinu zilizotumika katika tukio hilo zinawiana na
tukio la kumwagiwa sumu aina tindikali kwa mfanyabiashara aitwaye SAID S/O
MOHAMED@SAAD(42), mkazi wa Mikocheni maeneo ya Msasani katika jengo la Msasani
City Mall karibu na ubalozi wa marekani, ambaye ni mkurugenzi wa kampuni ya
Home Shopping Centre jijini Dsm. Tukio liliripotiwa Kituo cha Polisi Oysterbay Mwezi
wa saba mwaka 2013, OB/IR/7035/2013.
Mahojiano yanaendelea ili kubaini ushiriki wao
katika tukio tajwa pamoja na kushirikiana na Zanzibar na mikoa mingine ili
kubaini matukio mengine.
KUPATIKANA
KWA SILAHA MBILI RIFFLE MOJA, BASTOLA MOJA RISASI TATU NA MTUHUMIWA MMOJA
Jeshi la Polisi kanda maalum Dsm mnamo
tarehe 6/9/2013 majira ya saa sita kamili mchana huko maeneo ya Tandika
Magorofani (W) Temeke askari wakiwa doria walifanikiwa kupata silaha moja
bastola aina ya Browning AL.9 ikiwa na risasi tatu ndani ya magazine. –Awali
askari walikuwa doria katika maeneo hayo na kuitilia mashaka pikipiki moja aina
ya Boxer rangi nyekundu ambayo haikusomeka namba ikiwa na watu wawili, na pindi
watu hao waliposimamishwa hawakutii amri ya kusimama na badala yake waliongeza
mwendo, Na ndipo walipofika maeneo ya mtaa wa Bububu abiria aliyekuwa nyuma
alidondosha mfuko mmoja wa plastiki ambao baada ya askari kuupekua walikuta silaha
hiyo, Msako mkali unaendelea wa kuwatafuta watu hao wanaosadikiwa kuwa ni
majambazi.
Katika
tukio lingine mnamo tarehe 8/9/2013 majira ya saa kumi na moja jioni maeneo ya
Yombo Dovya CCM(w) Temeke, Jeshi la Polisi kanda maalum lilifanikiwa kumkamata
mtuhumiwa mmoja MFAUME s/o SAID (24) mkazi wa Mtwara akiwa na silaha moja aina
ya Riffle yenye namba 181531 akiimiliki kinyume cha sheria.Mtuhumiwa anaendelea
kushikiliwa kwa mahojiano zaidi.
KUKAMATWA KWA MAJAMBAZI WATATU AKIWEMO MWANAMKE
WANAOKABA NA KUPORA PIKIPIKI
Jeshi la
Polisi Kanda Maalum DSM mnamo tarehe 17/10/2013 saa moja na dakika arobaini
huko maeneo ya Coco beach(w) Ilala, mlalamikaji Joseph s/o Kilian(24)mkazi wa
kawe ukwamani akiwa ameegesha pikipiki
yake no.T178 CMC aina SANLG nyekundu
maeneo ya Coco beach walikuja watu watatu akiwemo mwanamke mmoja na kukodi pikipiki
yake ili awapeleke oysterbay shule, wakiwa njiani ghafla ilitokea pikipiki no.T
127 CJL aina ya SunLG nyekundu ikiwa na watu watatu abiria mmoja alimwambia
asimame, ghafla abiria wa kike aliyekuwa amempakia alimkaba shingoni kwa
kushirikiana na abiria wa pikipiki ya pili lakini dereva wa pikipiki hiyo
alifanikiwa kuondondoka chini akiwa amechomoa ufunguo na remote hivyo wezi hao
walishindwa kuiwasha pikipiki hiyo, wezi hao kuona hivyo waliamua kupanda
pikipiki yao na dereva huyo kuona hivyo aliwasha pikipiki yake na kuanza
kuwakimbiza akiwa njiani aliomba msaada kwa dereva wa gari ndogo Toyota Allex
na kumsaidia kuwafukuza wezi hao,
walipofika maeneo ya Palm Beach gari hiyo ilifanikiwa kuwagonga kwa
nyuma na wao kuanguka chini na Polisi walipata taarifa ya tukio hilo
wakishirikiana na polisi jamii waliokuwa karibu na kufanikiwa kuwakamata
watuhumiwa 3 ambao ni: 1.Ramadhani s/o Saidi (20) mkazi wa Mbagala
Saku,2.Maulidi s/o Ridhiwani (20) mkazi wa Mbagala Charambe,3.Siwema d/o ally
(20) mkazi wa Tandika Kichangani, Watuhumiwa wanashikiliwa kituo cha Polisi
Salender Bridge kwa mahojiano mara upelelezi utakapokamilika watapelekwa
mahakamani.
KUKAMATWA KWA WAHAMIAJI HARAMU KUMI NA SABA WA SOMALIA NA ETHIOPIA
Jeshi la Polisi kanda maalum Dsm mnamo
tarehe 6/09/2013 majira ya saa tano na nusu asubuhi huko maeneo ya Kipunguni
‘A’ katika msako endelevu wa kuwatafuta wahamiaji haramu wanaoishi nchini bila
vibali Polisi wakiwa doria walifanikiwa kuwakamata watu saba ambao ni raia wa
Somalia wanaoishi nchini kinyume na taratibu za kisheria.Watu hao ni 1.KURUMIE
s/o ABDALLAH (28) msomali na mkazi wa Kariakoo, 2.FARAGH s/o ISACK (22) msomali
mkazi wa Kariakoo 3.SAHLAL s/o ABDI (34)
msomali mkazi wa Kipunguni ‘A’ 4.MOHAMED s/o MAHMUD (42) msomali mkazi wa Gongo
la Mboto, 5.FARAGHA N s/o DAHIR (22) msomali mkazi wa Kawe
Beach,6.ABDULKADIR s/o HASSAN (21)
msomali mkazi wa Kipunguni ‘A’,7.MOHAMED s/o MUHAMED (21) msomali mkazi wa
Kipunguni ‘A’ watu hao watakabidhiwa idara ya uhamiaji kwa hatua zaidi za
kisheria.
Katika tukio lingine Jeshi la Polisi kanda
maalum Dsm mnamo tarehe 8/10/2013 majira ya saa moja asubuhi huko maeneo ya
Changanyikeni askari wakiwa katika doria walifanikiwa kuwakamata watu kumi
ambao ni raia wa Ethiopia wanaoishi nchini bila kibali kinyume na taratibu za
kisheria.Watuhumiwa hao ni 1.ELAMU s/o ABDUL (23), 2.EBEBE s/o GEBREMIKAL (32),
3.DINKAYO s/o DETAMO (30), 4.DESTA s/o SHANDE (25), 5.TUMISIDO s/o BASORE (20),
6.KESEYE s/o SHIGUTE (29), 7.DANIEL s/o LANDABO (25), 8.TSIGAYE s/o TADESA
(25), 9.BIRIHANI s/o MACHULA (22), 10.BEKELE s/o CHUFAMO (25). Watuhumiwa hao
wote wanaendelea kuhojiwa ili kubaini watu wanaofanya biashara hiyo haramu ya
kuwasafirisha pamoja na msako mkali
wa kuwabaini whamiaji wengine wote wanaoishi nchini bila
vibali maalum ili sheria ifuate mkondo wake.
KUKAMATWA
KWA MATAPELI WATATU MMOJA AKIWA NA KITAMBULISHO BANDIA CHA IDARA YA USALAMA WA
TAIFA
Jeshi la Polisi kanda maalum Dsm mnamo
tarehe 8/10/2013 saa mbili kamili usiku huko maeneo ya Beko hotel, Kawe Maringo
askari katika ufuatiliaji wa tukio la kuleweshwa madawa kwa JACKLINE d/o
GACHANGA (34) mfanyabiashara mkazi wa Salasala na hatimaye kuibiwa cheni moja
ya dhahabu,pete moja ya dhahabu ,fedha taslimu TSHs 800,000/=,simu moja aina ya
nokia pamoja na laptop moja,askari walifanikiwa kuwakamata watuhumiwa wawili
ambao ni KENEDY s/o MAGIGE SAMWEL (35)
mkazi wa Tabata na TAKULA s/o ABDALLAH
(32) mkazi wa Mbezi Beach ambapo wote walitambuliwa na mlalamikaji JACKLINE. Aidha mtuhumiwa KENEDY s/o MAGIGE
alipopekuliwa alikutwa na kadi za benki za watu mbalimbali pamoja na
kitambulisho bandia cha usalama wa taifa. Watuhumiwa walipohojiwa wote
walimtaja mshiriki mwenzao KHALIFAN s/o MALEMA (37) mkazi wa Kimara ambapo
askari usiku huo walifanikiwa kumkamata akiwa na mzani wa kupimia dhahabu.Watuhumiwa
wote wanaendelea kushikiliwa na Polisi na pindi upelelezi utakapokamilika
watafikishwa mahakamani.
KUKAMATWA KWA WATUHUMIWA
(46), BHANGI, KETE (252), PULI (8), MISOKOTO (13) NA GONGO LITA (193)
Jeshi la Polisi Kanda maalum Dsm limefanikiwa
kuwakamata watuhumiwa 46, bhangi kete 252,
bhangi puli 8,bhangi misokoto 13 na
gongo lita 3 , katika operesheni
endelevu ya vita dhidi ya madawa ya kulevya iliyoanza tangu 11.10.2013 hadi tarehe … katika maeneo mbalimbali ya jiji la DSM.
Watuhumiwa hao ni SAID S/O ABDALLAH (40)
ALLY S/O ABDALLAH (42), MUHIDI S/O HAMAD (22), MOUHAMED S/O OMAR (25), SELEMAN
S/O SHABANI (33),SALUM S/O ISMAIL (25), SHABAN S/O OMAR (32), REHEMA D/O MUNGI
(26), OMAR S/O MANDA (21), HEMED S/O ABDALLAH (20), FATUMA D/O MUOHAME (20),
MAWAZO S/O JUMANNE (37), KUDRA D/O SAID
(41), YASIN S/O JAFAR (30), MOUHAMED S/O SALUM (26), ANGELBERT S/O
DONARD (29), SHARIZ S/O ALLY (18), JUMA
S/O SAID (40), pamoja na watuhumiwa
wengine (85), watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani upelelezi utakapokamilika.
RAI
MMOJA RAIA WA SOMALI AKAMATWA NA NYARAKA ZA SERIKALI
Jeshi la polisi kanda maalum DSM mnamo
tarehe 18/10/2013 majira ya saa nne kamili usiku huko mwananyama A walifanikiwa
kumkamata raia wa Somali aitwaye JAMALI S/O IBRAHIMU(42) ambaye alikuwa akiishi
kwenye nyumba mmoja ya wageni iitwayo
MRANGI GUEST HOUSE, baada ya polisi kupata taarifa hizo walifuatilia na
kumkamata mtuhumiwa huyo akiwa na nyaraka za serikali kama ifuatavyo;
1.Form
no.130 za maombi ya makazi
2.Stakabadhi
21 za malipo ya vibali vya makazi
3.Nakala
8 za hati za kusafiria zenye picha za waombaji ambazo ni raia wa kisomali
4.Bahasha
moja yenye picha mbalimbali za waombaji ambao ni raia wa kisomali.
Aidha katika mahojiano mtuhumiwa anadai
anaishi katika nyumba hiyo ya wageni kwa kipindi cha miaka mitatu, ambapo awali
alikuwa akiishi kwa msomali mwenzake iliyopo mwananyamala ambapo imekwisha
uzwa, kuhusu uhalali wake wa kuishi nchini, kibali alichokuwa nacho cha uhalali
wa kuishi hapa nchini kimeisha muda wake tangu tarehe 08/08/2013 mahojiano
zaidi yanaendelea ili kuweza kubaini mtandao mzima anaoutumia na kupata nyaraka
hizo za wizara ya mambo ya ndani idara ya uhamiaji.
POLISI
KUIMARISHA ULINZI MKALI WAKATI WA MECHI YA LIGI KUU YA VODACOM
KATI YA SIMBA NA YANGA
UTAKAOFANYIKA TAREHE 20/10/2013
Jeshi
la Polisi kanda maalum Dsm kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na
usalama tumejipanga ipasavyo kuhakikisha mchezo huo wenye mvuto mkubwa kwa
mashabiki wa Tanzania, Nchi za Afrika Mashariki na Afrika nzima kuchezwa katika
hali ya usalama.
Aidha
tunaomba wananchi wasiwe na shaka yeyote ya kiusalama na pia watupe ushirikiano
wa kutoa taarifa kwa jambo lolote watakaloliona kuwa linaweza kuwa chanzo cha
uvunjifu wa amani kwa kipindi chote watakapokuwa nje au ndani ya uwanja.
Taarifa
hizo zitafanyiwa kazi haraka na kuwachukulia hatua wale wote watakaokuwa
wamehusika katika tukio husika kulingana na sheria za nchi/kanuni za usalama za
shirikisho la soka duniani (FIFA Safety Guidelines).
Vile
vile tunawasihi mashabiki wote wasije na vitu vyovyote ambavyo vinaweza
kutumika kama sila silaha (mfano soda za chupa na makopo ya maji, vipande vya
chuma, visu, mawe, au silaha za moto na vitu vya milipuko) vitu hivyo ni hatari
pindi ikitokea vurugu na kinyume na kanuni za usalama za FIFA.
Aidha
katika kuhakikisha watu wanaingia wakiwa salama tutafanya upekuzi katika
milango yoye ya kuingilia kwa kutumia mashine za kisasa(Metal Detector) na kuwachukulia hatua mashabiki watakaokiuka
agizo hilo.
Kutakuwa
na ulinzi katika majukwaa na askari na walinzi wasaidizi (stewards) wa kutosha
katika majukwaa yote kuhakikisha usalama unakuwepo kwa kipindi chote.
Tunawakumbusha mashabiki kuwa wastaarabu kwa kukaa majukwaaa yanayoendana na
aina/thamani halisi ya tiketi walizokata na si kuvamia maeneo ya VIP. Pamoja na
kuimarisha ulinzi wa ndani na nje ya uwanja (Inner and Outer
Perimeter Security measures) tutatumia
kamera za CCTV ili kufuatilia mienendo ya matukio yote.
Pia
barabara ya uwanja wa Taifa itafungwa kwa muda ili kupunguza foleni zisizokuwa
za lazima, pia magari hayataruhusiwa kuegeshwa katika eneo hilo na badala yake
watakaopenda kuja na magari watafute maeneo mengine salama ya kuegesha magari
yao.
S. H. KOVA – CP
KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAAM
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni