Jumatatu, 4 Novemba 2013

WEKUNDU WA MSIMBZI SIMBA WAANGUKIA PUA

Katibu mkuu wa mabingwa wapya wa ligi kuu soka nchini Kenya George Bwana ameukata mzizi wa fitna na kubainisha wazi kocha wao aliowapa ubingwa msimu huu Bobby Williamson haendi popote bado na wataendelea kuwa nae kwa misimu mingine ijayo.
Saa 24 zilizopita Kocha huyo wa zamani wa timu ya taifa ya Uganda amekuwa akihusishwa na taarifa za kuja kuinoa timu kutoka nyumbani Tanzania ambao ni mabingwa wa zamani wa ligi kuu soka ya Tanzania bara wekundu wa msimbazi Simba.
Bwana amekiri kumalizika kwa mkataba wa mwaka mmoja wa kocha huyo pamoja na mambo mengine amebainisha maamuzi ya klabu kumuongezea mkataba mwingine kuelekea kwenye msimu ujao wa ligi nchini humo.
Bwana ameongezea kuwa yote yanayoandikwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari vya Tanzania kuhusiana na kocha huyo ni maneno tu yenye lengo la kuwavuruga.
Kama itakumbukwa hapo jana wakati wakikabidhiwa ubingwa wao wa ligi msimu huu, kocha wa Gor Mahia Bobby Williamson aliamua kumzawadia medali yake Patrick Osewe ambaye ni dereva wa gari linalotumika kubeba kikosi cha Gor Mahia.
Bobby amesema kuwa dereva huyo ni sehemu ya ushindi walioupata hivyo ana kila sababu ya yeye kujivunia kazi kubwa ya kuwafikisha salama dimbani ambako wanakwenda kuchukua alama 3 muhimu zilizowaweka kileleni.
Gor Mahia rasmi walizawadiwa kikombe chao cha ubingwa wa ligi msimu huu mara baada ya kumalizika kwa mchezo wao wa raundi ya 29 ambapo walikubali kichapo cha magoli 2-0 toka kwa KCB.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni