Jumatatu, 4 Novemba 2013

WATATU KUFIKISHWA MAHAKAMANI KUVURUGA MCHEZO KATI YA SIMBA DHIDI YA KAGERA SUGAR




Jeshi la polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam inawashikilia watu watatu kwa kosa la kufanya vurugu wakati wa mchezo wa ligi kuu soka ya Tanzania bara kati ya wekundu wa msimbazi Simba dhidi ya Kagera Sugar mwanzoni mwa juma lililopita, mchezo uliomalizika kwa mabomu ya machozi kupigwa baada ya timu hizo kwenda sare ya kufungana bao 1-1.
Kamishna wa polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam Suleimani Kova amesema kuwa watu hao watafikishwa mahakamani wakati wowote kutoka sasa nab ado wanaendelea na msako kuwabaini wengine ambao pia wamehusika katika vurugu hizo.
Kila mtu na njia yake
Mapengo kibaoooo
Ona mambo hayoooo
Taarifa ya kulaani vurugu


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni