Ligi
ya mabingwa barani Afrika ambapo jana kumepigwa fainali ya pili, ikishuhudiwa
Al Ahly ya nchini Misri ikifanikiwa kutetea kikombe chake baada ya kuwachapa
Orlando Pirates kutoka Afrika kusini magoli 2-0.
Ahly,
imeandika historia nyingine jana ikibeba taji la ubingwa wa Afrika kwa mara ya
nane ikiwa imeshinda ushindi wa jumla magoli 3-1, magoli mawili kwenye mchezo
huo wa hapo jana pamoja na ile sare ya bao 1-1 katika mchezo wa fainali ya
kwanza iliyopigwa huko Soweto Afrika kusini.
Shukrani
za pekee katika ushindi huo wa magoli mawili umuendee mkongwe Mohammed Abutrika
aliyetikisa nyavu dakika ya 54 pamoja na Ahmed AbdulZahir dakika ya 78.
Kikosi
hicho kimezawadiwa dola za kimarekani Millioni 1-5 na wanataraji kuliwakilisha
bara la Afrika kwenye michuano ya kombe la dunia la vilabu itkayopigwa kuanzia
Disemba 11 hadi Disemba 21 mwaka huu nchini Morocco.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni