Timu ya taifa ya Ethiopia wanataraji kukwea pipa
alhamis hii kuelekea Calabar kukamilisha kibarua chao cha mtoano mchujo wa
kuomb la dunia dhidi ya timu ya taifa ya Nigeria The Super Eagles.
Shirikisho la mpira wa miguu la Ethiopia limesema
kuwa wataondoka kuelekea Calabar wakiwa na mashabiki ili kukipa hamasa kikosi
chao kuelekea katika mchezo huo muhimu kwa taifa lao, na tayari msafara wa
awali wa kikosi hicho umeshawasili huko Nigeria ukiongozwa na katibu mkuu wa
shirikisho kuhakikisha kila kitu kinakuwa sawa kabla ya mchezo wa hapo
jumammosi.
Ethiopia walipoteza mchezo uliopita kwa magoli 2-1
dhidi ya Nigeria mchezo uliopitwa Adis Ababa nchini humo na sasa wanahitaji
ushindi wa magoli 2-0 kujihakikishia tiketi ya kushiriki fainali hizo mwakani
nchini Brazil.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni