Contacts for Media:
Maurice Njowoka Gerald Ndalahwa Ndimila
Brand Manager Tanzania PR Manager
Coca-Cola Central, East & West Africa
Ltd Sonda Communications
Cell: 0688341201 Tel: +255783188181
mnjowoka@coca-cola.com
gerald@sondacom.co.tz
TANZANIA KUWA
MWENYEJI WA ZIARA YA KOMBE HALISI LA FIFA LA DUNIA 29/30 NOVEMBA, 2013
“Ziara ya Kombe la FIFA la Dunia na Coca-Cola” Kuwasili Dar
es Salaam Novemba 29 ikiwa ni sehemu ya ziara ya dunia
Coca-Cola kugawa tiketi bure kwa mashabiki wa soka jijini Dar
es Salaam ili kuwapa fursa ya kushuhudia Kombe halisi la FIFA la Dunia
Dar es
Salaam, Jumatatu, Novemba 4, 2013 … Kombe la FIFA la Dunia – kielelezo halisi na nembo
ya ubora wa soka duniani – litawasili jijini Dar es Salaam tarehe 29 Novemba
mwaka huu wa 2013.
Coca-Cola inalifanya Kombe la FIFA la Dunia 2014, kuwa
karibu zaidi na mashabiki wa soka na tukio kubwa kuliko fainali nyingine
zilizopita. Ziara ya Kombe la FIFA la Dunia na Coca-Cola litatoa fursa kwa
mashabiki zaidi ya milioni moja kushuhudia kombe halisi la FIFA la Dunia katika
nchi zao.
Hii ni ziara kubwa na ndefu zaidi ya kombe la dunia.
Ni ziara ya nchi 88 inayodumu kwa muda wa miezi tisa ambayo itajumuisha nchi 39
za bara la Latin Amerika ambako ndio bara mwenyeji wa fainali za kombe la dunia
2014 ilipo. Vile vile ziara hii itajumuisha nchi 50 ambazo hazijapata fursa ya
kuwa wenyeji wa ziara ya kombe la dunia.
Ziara ya kombe la dunia imeanzishwa kutokana na
ushirikiano wa aina ya pekee uliopo kati ya FIFA na Coca-Cola. Kampuni ya Coca-Cola ni mshirika wa FIFA wa
hali ya juu na ni moja ya washirika wa FIFA wa muda mrefu.
Akiongea wakati wa hafla rasmi ya kutanganza ujio wa
kombe la FIFA la Dunia nchini Tanzania, Meneja Mkazi wa Coca-Cola Tanzania Yebeltal
Getachew alisema kwamba ziara ya kombe la dunia itatoa wasaa adimu kwa maelfu
ya wapenzi wa soka jijini Dar es Salaam kuliona kwa karibu kombe halisi la
dhahabu la FIFA la Dunia. “Kupitia ziara
hii na promosheni nyingine kuelekea fainali za kombe la FIFA la Dunia 2014, Coca-Cola
itasheherekea hamasa ya soka na kujalibu kuzifanya fainali zijazo kuwa
shirikishi zaidi kuliko zilizopita,” alisema.
Wakati wa ziara ya kombe la dunia, mashabiki
watapata nafasi ya kufurahi na kuliona kombe halisi la FIFA la Dunia kwa
karibu. Tiketi zitatolewa na Coca-Cola kupitia promotioni mbalimbali.
Mashabiki pia watapata fursa ya kupiga picha na
kombe, kutazama video inayoonyesha matukio mbalimbali ya kihistoria ya kombe la
FIFA la Dunia na kufurahia burudani za kusisimua.
Ziara ya Kombe la FIFA la Dunia 2013 limezingatia
mafanikio makubwa ya ziara ya kombe hilo zilizofanyika mwaka 2006 na 2009 ambapo
mamilioni ya wapenzi wa soka walipata nafasi ya kuliona kwa karibu kombe hilo
ambalo ni zawadi ya thamani zaidi ya mpira wa miguu duniani.
Kombe la FIFA la Dunia huzawadiwa timu inayoshinda
fainali za kombe la dunia. Kombe hilo
lina urefu wa sentimita 36.8 (14.5 inches), uzito
wa gramu 6,175 (13.61 poundi) na limetengenezwa kwa dhahabu tupu (18-carat gold). Timu bingwa hushikilia kombe hilo hadi
fainali zinazofuata, baada ya hapo hupewa mfano wake mbalo siyo la dhahabu. Chini ya kombe hilo kuna kina leya mbili za malachite,
wakati kitako chake kinaonyesha washindi wa kombe la dunia tangu 1974.
Kampuni ya Coca-Cola
ni moja ya washirika wa muda mrefu wa FIFA, na ushirikiano huo ulikuwa rasmi
mwaka 1974 na kuwa mdhamini rasmi wa kombe la FIFA la Dunia mwaka 1978. Coca-Cola ilianza kuweka matangazo yake
kwenye viwanja vya Kombe la FIFA la Dunia tangu. Mwezi Novemba 2005, Coca-Cola na
FIFA waliongeza muda wa ushirkiano wao. Ushirikiano huo unaongezwa kuzingatia
masharti fulani fulani hadi 2022.
Ikiwa mshirika wa FIFA
wa vinywaji baridi, Kampuni ya Coca-Cola imepewa haki za udhamini katika
mashindano yote ya FIFA, ikiwa ni pamoja na Kombe la FIFA la Dunia na haki
pekee za kujitangaza.
Ziara ya
kombe la dunia inakuja kufuatia matukio makubwa ya kimichezo ambayo Coca-Cola iliyafanya
kuelekea kuelekea fainali za kombe la FIFA la Dunia, ikiwa ni pamoja na
mashindano ya vijana chini ya umri wa miaka 15 ya Copa Coca-Cola yaliyomalizika
hivi karibuni.
MWISHO
Meneja Mkazi wa Coca-Cola Yebeltal Getachew akitangaza ujio wa Kombe la FIFA la Dunia nchini Tanzania Novemba 29, 2013. Kushoto ni Mkurugenzi wa michezo nchini Bw. Leonard Thadeo. |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni