Jumatano, 26 Machi 2014

YANGA YAZIDI KUJIKITA KILELENI


 Vinara wa ligi kuu soka ya Tanzania bara waoka mikate wa Azam fc wamezidi kujikita kileleni mwa ligi hiyo wakifikisha alama 50 baada ya kuwatandika mgambo Jkt mabao 2-0 huko kwenye uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.

Hadi mapumziko milango ya timu zote ilikuwa migumu na iliwachukua Azam dakika 15 za kipindi cha pili kupata bao la kuongoza kupitia kwa mshambuliaji wake John Bocco Adebayor kabla ya Brian Umony kutumbukia tena wavuni na kuyafanya matokeo ya mchezo huo kumalizika kwa Azam kupata ushindi wa mabao 2-0.

Kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam nao mabingwa watetezi Dar es salaam Young Africans ilikuwa dimbani kukipiga dhidi ya maafande wa Tanzania Prisons Wajelajela kutoka mjini Mbeya.

Yanga wamefanikiwa kuchomoza na ushindi mnono wa mabao 5-0 mabao yaliyotupiwa wavuni na Emmanuel Okwi dakika ya 20, Mrisho Khalfan Ngassa dakika ya 37, Hamisi Kiiza dakika ya 68, 88 na Nadir Haroub Ally Canavaro dakika ya 78.

Kwa matokeo hayo Yanga wanaendelea kusalia kwenye nafasi ya pili wakifikisha alama 46 wakiwa na mchezo mmoja mkononi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni