Jumanne, 25 Machi 2014

CAF SET FOR BIG DRAW



Shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika CAF limeichagua April mosi mwaka huu kuwa ndiyo siku itakayofanyika zoezi la upangaji wa makundi ya ligi ya mabingwa barani Afrika pamoja na ratiba ya raundi ya pili ya 16 bora ya kombe la shirikisho.

Zoezi hilo kama kawaida litafanyika makao makuu ya CAF yaliyopo Cairo nchini Misri ambapo raundi ya pili hatua ya awali ya makundi ya klabu bingwa Afrika imepangwa kuchezwa kati ya March 28 hadi 30.

Kama ilivyoada zoezi hilo litaanzia na timu 8 ambazo zimefuzu kwenye hatua ya makundi na timu za kombe la shirikisho barani Afrika.

Nikikumbushia matokeo ya mkondo wa kwanza ya 16 bora mechi ambazo zilipigwa juma lililopita.
Mabingwa watetezi wa klabu bingwa Al Ahly ya Misri ilianza kwa kupokea kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Al Ahly Benghazi ya Libya, Zamalek ya Misri ilitoka sare ya kutofungana na Nkana fc ya Zambia wakati Sewe Sport ya Ivory Coast ikiichapa TP Mzembe ya Congo DRC mabao 2-1.

Horoya fc ya Guinea ilikubali kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Club Sportive ya Tunisia, Setif ya Algeria ikaichapa Coton Sport ya Cameroon goli 1-0, Ac Leopards ya Congo ikaenda suluhu ya bao 1-1 na Al Hilal ya Sudan wakati AS Vita ya Congo DRC ikiitandika Kaize Chiefs ya bondeni Afrika kusini mabao 3-0.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni