Jumatatu, 24 Machi 2014

MIDO RUES MISSED CHANCES

Baada ya kikosi chake kushindwa kuambilia alama tatu wakati wa mchezo wa hatua ya 16 bora klabu bingwa Afrika, kocha mkuu wa Zamalek ya nchini Misri Ahmed Mido Hossam bado anaimani timu yake inanafasi ya kusonga mbele kunako michuano hiyo.

Jumamosi iliyopita Zamalek ilijitupa dimbani huko nchini Zambia kucheza dhidi ya wenyeji wao Nkana FC ukiwa ni mchezo wa mkondo wa kwanza wa ligi ya mabingwa barani Afrika uliomalizika kwa sare ya kutofungana.

Mido amekipongeza kikosi chake kuwa kilicheza vizuri japo bahati haikuwa upande wao hivyo wanahitaji kutumia Baraka ya uwanja wa nyumbani wa El Gouna kuhakikisha wanapata ushindi wakati wa mchezo wao wa marudiano utakaopigwa mwishoni mwa juma hili.

Wakati huo huo Mido amewapongeza wapinzani wao Nkana FC kuwa walionesha kiwango cha hali ya juu na walistahili kupata ushindi lakini akatabahisha kuwa matokeo ya mchezo wa marudiano wasitarajie kama watapata nafasi hata ya kufanya shambulizi langoni mwa Zamalek kwakuwa wamejipanga kuhakikisha wanaumiliki mchezo kwa dakika zote 90.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni