Jumatatu, 24 Machi 2014

ASAMOAH GYAN CONTINUES TO ABSTAIN FROM GHANA PENALTY DUTIES



Nahodha wa timu ya taifa ya Ghana Asamoah Gyan amesisitiza kuwa ataendelea kuipigia mikwaju ya penalty timu yake The Black Stars wakati wa matuta lakini si wakati muhimu wa kuinusuru kubaki ama kuondolewa kwenye michuano ya kombe la dunia.
 Nahodha huyo alishauriwa na marehemu mama yake kujihadhari na upigaji wa penalty mara baada ya kutolewa kafara wakati akishindwa kuisaidia timu yake tutinga fainali za AFCON mwaka uliopita.
Alikosa penalty muhimu kwenye mchezo wa ufunguzi wa nusu fainali ambao walipokea kipigo cha goli 1-0 kutoka kwa Zambia tukio ambalo lilimpa wakati mgumu kutokana na maneno ya mashabiki ambayo yalimfanya ajiondoe kwenye timu ya taifa kwa muda.
Amesema kuwa kamwe hatarajii kujitolea kupiga mkwaju wowote wa penalty kwa timu yake ila ikilazimika kupiga penalty ambayo haitakuwa na madhara ya kuiweka kwenye wakati mgumu timu yake atapiga.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni