Kiungo wa
Ghana Kevin-Prince Boateng ataikosa hamasa ya mchumba wake mwanamitindo Melissa
Satta wakati timu yake ya Schalke 04 ikicheza dhidi ya Borussia Dortmund hapo
kesho.
Mwanamitindo huyo kutoka nchini Italia anataraji kujifungua ndani ya ndani
ya wiki tatu hivyo ameshauriwa kutumia muda miwngi kupumzika na si
kujichanganya kwenye mkusanyiko wa watu wengi.
Boateng amezoea kumuona mchumba wake akimshangilia uwanjani lakini safari
hii atalazimika kuikosa hali hiyo ila kunusuru mtoto wake azaliwe salama na
akiwa mwenye afya njema.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni