Kutokana na hali ya usalama kuwa
bado haijatengamaa nchini Libya, Uongozi wa chama cha soka cha Algeria
umejitokeza kutaka kuchukuwa nafasi ya kuandaa michuano ya kombe la mataifa ya
Afrika ya mwaka 2017.
Shirikisho la mpira wa miguu barani
Afrika CAF bado halijafanya maamuzi, kama michuano hiyo ihamishwe kutoka Libya
kupelekwa kwenye taifa lingine.
Waziri wa michezo wa Algeria Mohamed
Tahmi amesema kuwa wapo tayari kuandaa fainali za AFCON kama Libya watapokonywa
haki hiyo ya kuwa nchi mwenyeji kwa mwaka 2017.
Amesema kuwa nchi yake ina miundombinu
ya kutosha na yakuridhisha kufana kwa fainali hizo na wanaamini wana uwezo wa
kutosha wa kumudu mahitajio yote muhimu.
Aidha ameongezea kuwa wanasubiri
maamuzi ya CAF kama watabaki na msimamo wa kuipa Libya haki hiyo ama laaa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni