Michuano ya mwaka huu ya kombe la Kagame imesogezwa
mbele hadi mwezi August badala ya mwezi June kama ilivyoarifiwa hapo awali ili
kupisha kumalizika kwa michuano ya kombe la dunia itakayofanyika mwezi June
huko Brazil.
Katibu mkuu wa baraza la vyama vya soka vya Afrika mashariki na kati Nicolaus Musonye amethibitisha kuhusiana na hilo na kutanabahisha kuwa bado hawajaipata nchi mwenyeji wa kuandaa michuano hiyo.
Katibu mkuu wa baraza la vyama vya soka vya Afrika mashariki na kati Nicolaus Musonye amethibitisha kuhusiana na hilo na kutanabahisha kuwa bado hawajaipata nchi mwenyeji wa kuandaa michuano hiyo.
Amesema kuwa wapo katika mazungumzo na nchi za
Rwanda na Sudan kuona uwezekano wa kuandaa michuano hiyo ambayo walipanga
ifanyike mapema kabla ya kuanza kwa michuano ya kombe la dunia lakini kutokana
na timu nyingi kuwa bado wanakabiliwa na vibarua vya klabu bingwa pamoja na
kombe la shirikisho barani Afrika wameamua kuyasogeza mbele hadi mwezi August.
Michuano hiyo ambayo inafadhiliwa na Rais wa Rwanda
Paul Kagame, kwa mwaka jana ilifanyika Darfur nchini Sudan na kushuhudiwa
Vital’O kutoka Burundi ikitawazwa kuwa bingwa wakati timu kutoka nyumbani
Tanzania Bara zikijiondoa kushiriki michuano hiyo kutokana na hali ya usalama
ilivyo huko Sudan.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni