Jumatatu, 24 Machi 2014

NIGERIA COACH KESHI SAYS HE IS NOT WORRIED BY CRITICISM


Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Nigeria Stephen Keshi amesema kuwa kamwe hatokatishwa tamaa na maneno ya mashabiki pamoja na wadau wa soka ambao wamekuwa wakimbeza juu ya maamuzi ya kikosi chake.

Hajawahi kupoteza mbele ya wapinzani wengine wa Afrika kwenye kipindi cha miaka mitatu lakini bado kocha huyo anaonekana kujadiliwa zaidi kwa mabaya.

Lakini Keshi amekubali kuendana na hali hiyo ya maisha huku akiamini kuwa ni sehemu ya maisha na siyo wote watakaompenda.

Amesema hana wasi na hisia za watu juu ya kazi na wala hajali jambo lolote lile kwakuwa familia yake inampenda na inampa ushirikiano katika kufanya kibarua chake kwa ufanisi.

Nahodha huyo wa zamani wa The Super Eagles ambaye alijiunga na kikosi cha Nigeria mwaka 2011, amefanikiwa kurejesha hadhi ya soka la Nigeria kwa kufanikisha kutwaa kombe la mataifa ya Afrika mwaka jana pamoja na kuiongoza nchi hiyo kuwa miongoni mwa mataifa mbalimbali yatakayoshiriki fainali ya kombe la dunia mwaka huu wa 2014.

Licha ya mafanikio hayo, kwasasa hatma ya kocha huyo imeanza kuweka walakini kufuatia baadhi ya vyombo vya habari kuvujisha taarifa za ndazi za shirikisho la soka la Nigeria kuwa liko mbioni kumuajiri kocha mpya raia wa kigeni.

Akifunguka kuhisiana na hatma ya kibarua chake Keshi amesema kuwa kazi ya ukocha ni sawa na bahati nasibu ambayo siku unapata na siku unakosa, cha msingi anajivunia kazi kubwa aliyoifanya kwa kipindi chote alichoinoa timu hiyo na kama wataamua kumtumia na kumuajiri kocha mwingine yeye yuko tayari na kamwe hawezi kuwa na kinyongo.

Aidha ameongezea kuwa kama watu wameamua kuzungumza waache wazungumze na wala hawezi kuwazuia yeye ataendelea kufanya yake ikiwemo kujiongezea sifa zaidi ya kuwa kocha pekee kutoka barani Afrika kuyawezesha mataifa mawili kufuzu fainali ya kombe la dunia.

Kuelekea kwenye michuano ya kombe la dunia ya mwaka huu Nigeria imeangukia kundi F linalojumuisha timu ya Iran, Bosnia-Hezrgovina na Argentina.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni