Vinara wa ligi kuu soka ya Tanzania bara waoka
mikate wa Azam fc wamezidi kujikita kileleni mwa ligi hiyo wakifikisha alama 50
baada ya kuwatandika mgambo Jkt mabao 2-0 huko kwenye uwanja wa Mkwakwani mjini
Tanga.
Hadi mapumziko milango ya timu zote ilikuwa migumu
na iliwachukua Azam dakika 15 za kipindi cha pili kupata bao la kuongoza
kupitia kwa mshambuliaji wake John Bocco Adebayor kabla ya Brian Umony
kutumbukia tena wavuni na kuyafanya matokeo ya mchezo huo kumalizika kwa Azam
kupata ushindi wa mabao 2-0.
Kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam nao
mabingwa watetezi Dar es salaam Young Africans ilikuwa dimbani kukipiga dhidi
ya maafande wa Tanzania Prisons Wajelajela kutoka mjini Mbeya.
Yanga wamefanikiwa kuchomoza na ushindi mnono wa
mabao 5-0 mabao yaliyotupiwa wavuni na Emmanuel Okwi dakika ya 20, Mrisho
Khalfan Ngassa dakika ya 37, Hamisi Kiiza dakika ya 68, 88 na Nadir Haroub Ally
Canavaro dakika ya 78.
Kwa matokeo hayo Yanga wanaendelea kusalia kwenye
nafasi ya pili wakifikisha alama 46 wakiwa na mchezo mmoja mkononi.