Shirikisho la soka barani Afrika CAF limetoa orodha
ya mwisho ya wachezaji 10 wanaowania tuzo ya mwanasoka bora Afrika na na
wengine watano wanaowania tuzo ya mwanasoka bora wa Afrika anaekipigia ndani ya
bara hilo.
Majina ya wachezaji 10 wanaowania tuzo ya mwanasoka
bora ni Mohammed Abutrika kutoka Misri, Pierre Emerick Ubamiyang kutoka Gabon,
Didier Drogba na Yaya Toure kutoka Ivory Coast, Emmanuel Emenike, Vicent
Enyima, Ahmed Mussa na John Mikel Obi wote kutoka Nigeria, Asamoh Gyan kutoka
Ghana na Jonathan Pitroipa kutoka Burkina Faso.
Katika orodha ya wachezaji Watano wanaokipigia ndani
ya Afrika Mohammed Abutrika ametinga kwa mara nyingine huku mshambuliaji kutoka
nyumbani Tanzania anaekipigia ndani ya TP Mazembe ya Congo Mbwana Ally Samatta
ametupwa nje ya kinyang’anyiro na nafasi yake imechukuliwa na Rainford Kalaba pamoja
na Tresor Mputu kutoka kwenye klabu ya TP Mazembe huku Nigeria ikipata
muwakilishi mmoja ambaye ni Sunday Mba.
Hafla ya utoaji Tuzo itafanyika January 9 mwakani
huko Lagos nchini Nigeria.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni